Friday, March 02, 2007

WAMESIKIA KILIO CHETU, SASA TUPO MTANDAONI!!!!!

Niliwahi kukuandikeni kuhusu kutokuwapo kwa huduma ya kisasa ya intanet hapa katika chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere, kwa sasa hii leo inaweza kuwa ni historia kwani kwa muda huu ninapokuandikia nimo ndani ya chumba ambacho zamani kilikuwa kimefungwa kwa makufuri makubwa ya solex na milango ya vyuma yakihifadhi kompyuta, ninakuandikia habari hii huku mwalimu wa somo akiwa pembeni.

Wanachuo sasa hatuna haja kwenda 'ferry' ili kupata huduma hii muhimu ambayo baadhi ya 'watu' wanaiona kama ni ya anasa.

lakini kikubwa kinachoonekana hapa ni ratiba ya kuingia madarasani kwani kuna baadhi ya wanafunzi wanaamua kushinda 'lab' wakiamini mtandao ndo kila kitu, labda ni 'ugeni'.
Tusubiri tuone mabadiliko ambayo yameendana kabisa na uongozi mpya wa chuo

No comments: