Monday, October 30, 2006

MASO SASA MTANDAONI

Kwa muda mrefu sasa wanachuo wa MNMA wamekuwa wakikosa ni wapi wanaweza kusemea na maoni yao kueleka kwa wengine.

MASO serikali ya wanafunzi imeanza kazi ya kuwaunganisha wanafunzi waliosoma katika chuo hiki na wale wanaosoma sasa kwa e mail ifuatayo;

masomnma@yahoo.com

Ukiwa kama mdau wa serikali ya wanafunzi hapa MNMA unaombwa kuchangia kwa kushiriki kuandika mambo mbalimbali kwa kutumia anuani hiyo. Kumbuka uwanja mpana unakuja hivi karibuni

Sunday, October 29, 2006

MASO-MNMA NA TEKNOLOJIA YA BLOG

Msomaji wa machweo, usitishike kusoma kchwa hapo juu kwani nahisi ni kigeni sana kwako.
MASO-MNMA ni kifupi cha jina la serikali ya wanafunzi wa chuo cha kumbukumbu ya mwl. Nyerere.

Kwa mwaka huu wa masomo2006/07 maso iko chini ya rais Hasaan Masudi, na moja ya malengo makubwa ya serikali hii ni kuwaunganisha wanafunzi wote si wa memorial tu bali wa dunia nzima kwa kuingia katika dunia ya blog.

Kwa sasa tegemea makubwa toka katika blog hii itakayokupa mengi toka kwa wanzuoni wa MNMA. Blog hii itakuwa chini ya wizara ya habari inayoongozwa na Obe Mashauri
MRAMBA, BILA MWALIMU, NYERERE NI MTU MWINGINE


Hivi karibuni waziri Mramba aliutangazia umma wa watanzania kuhusu madiliko katika kiwanja cha kimataifa cha dar es salaam. mabadiliko hayo ni katika sehemu moja muhimu sana nayo ni ya utambulisho wa mgeni kujua hapa ni wapi na mwenyeji kujivuna kwa kuwa na utambulisho huo.

Mramba na timu yake wanasema kwamba kutokana na sababu za taratibu za kimawasiliano, kiwanja cha ndege cha dar maarufu kama Mwalimu Nyerere international airport sasa kitakuwa kinaitwa Nyerere IA.

mmmh! hii kweli ndo kasi mpya inayohubri mabadiliko makubwa kwa watanzania na mabadiliko haya ndiyo tunayoyaona sasa, yaani watu kwa utashi wao tu wanaamua kubadili jina la kiwanja hiki kwa kuwa tu wazungu hawawezi kutamka jina mwalimu!

Huu ni ulimbukeni na kama anavyosema msanii wa parapanda Mputo katika ghani zake 'salamu zangu' kuwa msikihubiri kiswahili kwa kukitukuza kingereza, kwani kwa miaka yote jina la nyerere shurti lianze na mwalimu na hapo kila mtu duniani hatohoji kwamba huyu mwalimu ni nani. Alijulikana dunia nzima na harakati zake zinazofundishwa kila kona ya dunia hii.

Kuondoa jina mwalimu kisa tu kuna wachache wanapata shida kutamka ni sawa na kusema JFK IA libadilishwe na kuwa unavyotaka wewe. Mbona kuna majina ya viwanja vya ndege si Africa tu bali na sehemu mbalimbali duniani ni magumu si kutamka tu bali hata kuandikwa lakini ndiyo yanayobeba viwanja hivyo.

wanamachweo wanategemea waziri na wizara yake itafanya kama watanzania wanavyohitaji bila kuhoji kwa nini!

na kwa kumalizia kwa watu wenye mawazo kama ya Mramba ni kwamba huwezi kusema nyerere ukimaanisha mwl Nyerere tunayemfahamu sisi watanzania na watu wote duniani, labda kama mnataka kutueleza kuwa jina hilo halina maana sasa.

Monday, October 09, 2006

CHUO KIMEPATWA MSIBA!!!!!

Ni asubuhi ya tarehe 09/10/2006 kilamwanachuoamekwisha jiandaa tayari kwakwenda darasani,mara rais wa serikali ya wanafunzi wa chuocha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ndugu Hassan J. Masoud anaitisha kikao na wanafunzi wote katika ukumbi wa mikutano.

Hili si jambo la kawaida kwani inaashiria kuna kitu kikubwa wanachuo wanapaswa wahabarishwe, naam, maskio ya kila mmoja yanasubiri nini kitasemwa pale ukumbini na kila mtu yupo kimya. Rais anaanza kuongea ni tangazo la msiba, Msiba mzito wa kaimu naibu mkuu wa chuo ndugu O. K. Temwende

Ni majonzi chuoni na kila mtu haamini kwamba mtu waliyekuwa naye siku moja kabla ametutoka. Kila mmoja anasema analojua na aliloona, wengi tuliongea naye siku ya ijumaa kuhusu tatizo la ada, wengine wakawa naye katika bar ya chuo.

Najua wapo wengi wanaoweza kusema mengi juu ya mwanataaluma huyu, nami pia kwa muda wa kama mwaka mzima tangu nijuane naye chuoni nina mengi yakukumbuka na kujiuliza na kama si kukilaum kifo kwa ukatili uliofanya juu ya mwanazuoni huyu na kada mwaminifu wa chama cha mapinduzi.

Temwende alisoma shule ya Ndanda sekondari zamani sana ikiwa chini ya wabenediktini wa Ndanda shule ambayo miaka ya 90 ilichukuliwa na serikali ambapo nami nilipata elimu ya juu ya sekondari miaka ya 2000. Alipata elimu ya juu katika vyuo mbalimbali vya ndani na nje ya nchi na ninachoweza kukumbuka ni pale alipokwendakuchukua masomo ya juu katika moja ya nchi zakisosharist akiwa na A. Mrema kada mwingine wa CCM enzi hizo ambaye sasa ni Rais wa TLP

Darasani marehemu Temwende atakumbukwa kwa kuwa muwazi na siku zote alisistiza umakini na kushirikiana katika shughuli za kimasomo, alisikiliza tatizo la kila mmoja na hakusita kutoa ushauri kwa yeyote aliyeuhitaji.

Marehemu Temwende aliyezaliwa mkoa wa Mttwara alikuwa ni mwandishi mzuri wa makala na kwa wasomaji wa magazeti na hususani wasomaji wa magazeti ya propaganda ya CCM watakumbuka makala zake nzito zilizokuwa zikitolewa wakati Tanzania ilikuwa katika kipindi cha kusaka maoni uwepo wa vyama vingi katika nchi hii.

Temwende alikuwa na dhamana kubwa hapa chuoni na jinalake litabaki katika kumbukumbu za chuo kwani ni yeye aliyeongoza jopo la wahadhiri wa MNMA katika mchakato wa kukifanya chuo kuwa chuo kikuu na hivyo kutoa shahada. Alifanikiwa na matunda yake hakuna anayeyatilia shaka kwani yanaonekana. Alikuwa ni mtu wa vitendo kuliko porojo na propaganda zisizozalisha.

Kuna mengi ya kuandika juu ya marehemu Temwende aliyefariki wakati akiwa njiani kupelekwa hospitali baada ya kuugua ghafla na kukosa pumzi akiwa nyumbani kwake maeneo ya kigamboni jirani tu na ofisi zake za kazi.

Imetangazwa tuna mapumziko ya msiba lakini mambo aliyoyanya marehemu juu ya chuo na kwa kila mmoja aliyemzunguka hayatafutika na hata wengine kujilamu kwamba kwanini amekubali kufa kama padri Karugendo alivyomlaum profesa S. Chachage kwa kufa ilhali kazi waliyokuwa wameipanga kuifanya haijakamilika na kwa kuwa maisha yanaendelea, kila mtu baadaye atakuwa na furaha na pale Temwende alipokomea basi ndipo tutakapoanzia.

Bwana Alitoa na Bwana Ametwaa

Pumzika kwa Amani mpendwa wetu Omar K. Temwende