Monday, August 07, 2006

KIKWETE KAPOTOSHWA KUHUSU 'MAPANKI'

Watu wanayala sana na hao sato anaowasema wanaliwa na watu wenye uwezo kama wale waliompotosha kwa kusema kuwa wakazi wa mwanza hawali mapanki, wasaidizi wake wamemwingiza mkenge kwa nia tu ya kulinda vibarua vyao.

Mapanki ndo kitoweo cha wengi hasa waliovijijini.

Hii ndo hulka ya viongozi wengi, wanafikiri wao wanapokula vizuri na kusaza nasi twala na kutabasamu.

Sauper hajakosea hata kidogo kila alichokionyesha ni sahihi kwa sisi tunaoijua mwanza na vijiji vyake

Saturday, August 05, 2006

MAKAHABA TUWAFUKUZE, AU TUWAPE MITAJI WASITEGEMEE MIILI YAO?

Swali hili linatokana na hatua aliyoichukua mkuu mpya wa mkoa wa Dar es salaam bwana Kandoro.
Mkuu huyu baada ya kupewa rungu la ukuu wa mkoa muhimu wa kibiashara nchini tanzania alikimbilia maeneo ya manzese uwanja wa fisi na kuwatimua mabinti wadogo wanaofanya biashara ya kuuza miili (yeye anaiita ukahaba).

Siungani na watu wanaoshabikia kuwepo kwa mabinti hawa maeneo haya kwani licha ya kuwa umalaya/ukahaba si kitu kizuri kwa dunia ya sasa yenye gonjwa la ukimwi lakini wengi wa mabinti hawa ni wasichana wadogo kiumri(wengi wako chini ya miaka 18 miaka ambayo ni ya mtoto kuwa shule akitafuta elimu).

Sasa wamefukuzwa maeneo haya na wengine wamefikishwa mahakamani ambako mahakama imewaachia kwa kuwaona kuwa hawana hatia (ushahidi ni mgumu zaidi ya kumfungulia mtu mashtaka ya uzururaji). Kwa maana hiyo mabinti hawa wamefukuzwa toka maeneo yao na kutakiwa waondoke kwenda haieleweki wapi na wakafanye nini kwani sasa hawatakiwikujihusisha na umalaya/ukahaba tena.

Sielewi kama mkuu wa mkoa alikuwa anatafuta jina katika kurasa za mbele za magazeti yetu ama ni kasi mpya na nguvu mpya!

Unaweza kujadili suala hili, je kuwafukuza hapo ndilo suruhisha au suluhisho ni kuwaandalia mbiu nyingine za maisha kama KIWOHEDE wanavyofanya pale Buguruni. Pia ni lazima jamii ijue kuwa si Uwanja wa Fisi tu kunakofanyika uchafu huu, ni sehemu nyingi sana hapa dar na katikamiji mikubwa mingine kama Mwanza, Mbeya na Arusha
KANDORO NA WAKAZI WA MABONDENI NANI ZAIDI

Wakati akiwaapisha wakuu wapya wa wilaya za jiji la dar aliwataka kuhakikisha kuwa wanafanya kazi zao na kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa katiba. Huu kila mmoja anauelewa ili alinde kitumbua chake

Lakini amewakasirisha wakazi wa mabondeni ambao wamekuwa ni sugu na mara zote wameishinda serikali mahakamani kuhusu suala la kutoka katika maeneo haya hatari hususani maeneo ya jangwani.

Kilichonifanya niandike jambo hili ni ile kauli ya wakazi wa jangwani kwanza kumhusu Kandoro kama yeye na yeye kama mkuu wa mkoa, jiji la dar

Wengi walimweleza kama mgeni ambaye hata mjini hajakaa halafu anaanza kuwaletea longolongo wakati wao wamekuwa pale kwa miongo na watoto wao wanasoma muhimbili primary huku wakipata huduma ya uhakika ya matibabu toka hospitali ya taifa Muhimbili halafu leo Kandoro apange kuwaondoa!

Mgosi (Makamba) kashindwa atakuja yeye! tusubiri tuone kwani kasi aliyokuja nayo ya kuwatimua mabinti pale uwanja wa fisi inaweza kuwa juu ya wakazi wa mabondeni