Wednesday, May 24, 2006

NYERERE 'FEES' INAPANDA! UMEJIANDAA!!!!!!!!!

Huu sio kama ni uzushi bali ni utabiri halisi.

Chuo kimeamua kuongeza ada kwa wanafunzi wa diploma kisa eti wanatoa mafunzo ya komputa.

kweli jina la Nyerere sasa linatumiwa kibiashara

Nitakuandikia tena kwani kama watu tshs 600,000/= nanga inapaa itakuwa hii 800,000/= wanayopanga au ni kwa ajili ya masirahi binafsi ya kujilimbikizia pesa kwa mgongo wa wavuja jasho!!

tangazo hili likitolewa hakika mwalimu atajigeuza alipopumzika

More 2 come
Jamani, nimekuwa nikiwaza na kuwazua; Ni nani mfanyakazi bora katika ofisi zetu Tanzania?

Nauliza hivi kwa kuwa kila ifikapo tarehe kama ya leo kila mwaka, ofisi huwa zinahaha kutangaza wafanyakazi bora. Sijui wanatumia vigezo vipi.
Muda wote wachapakazi ndo wanakosa nafasi hizo na wanaopata ni wale wanaopendwa na wanaowateua; iwe manajimenti, ofisa mtendaji mkuu na wote wanaofanana na hao.
Sasa mimi nasema hakuna cha mfanyakazi bora wala nini. Wote n i watumishi tu na mtindo huo wa kuwepo wafanyakazi bora unadumaza utendaji wa kazi wa watu wengine na ndiyo maana nchi zetu haziendelei.
Nimemaliza

Tuesday, May 23, 2006

NAGOMBEA!!

Unashangaa, huu ndo ukweli ninagombea hata kama hakuna katiba ya kuongoza uchaguzi huu,

Naomba kura zenu katika nafasi ya michezo, kwani mimi nina uzoefu wa michezo yote ya ndani na ya nje
UCHAGUZI BILA KATIBA!!!

Usije ukafikiri ninachokuandikia hapa ni utani. 'Kaimu' rais wa MASO ametoa tangazo la kuwataka wale wote wanaotaka kuingia katika mchakato wa uchaguzi wa serikali ya wanafunzi hapa chuoni basi wachukue fomu katika ofisi za MASO!

Kila mmoja maeliona tangazo hilo lenye sahihi tu ya rais bila muhuri wa MASO yaani kwa ufupi kama usipokuwa makini tangazo limekaa kama barua tu unayoweza kumwandikia shangazi yako. Kila mtu anajiuliza hivi kweli uongozi hauna muhuri na kama hauna muhuri na kama hauna basi huu ni uhuni na haupaswi kuwepo.
WALIOCHELEWA WAMESAMEHEWA!!!!!!!!!


Juzi nilikuandikia kuhusu suala la wanachuo wachache waliokuwa wamechelewa na chuo kupitia kwa dean! wakaamriwa wafukuzwe na kama watapenda basi warudia mwaka wa masomo.

Wengi wa hawa waliochelewa ni wanafunzi wa mwaka wa pili ambao ni kama wamebakiza siku 26 wamaliza kozi na kutunukiwa diploma yao kama watakuwa wamefaulu.

Mapema leo asubuhi wamepewa barua za kuondoshwa chuoni zikiwa zimesainiwa na kaimu wa naibu wa mkuu wa chuo.Barua hizo hazina rejea hata moja na kuonyesha kosa la mhusika, zimemshangaza kila mmoja hata yule asiyekuwa na elimu ya sheria kifupi ni kwamba zinakanganya sana.

mkanyiko huu hauishii kwenye barua tu kwani wakati wa kipindi cha tatu leo mchana Naibu wa mkuu wa chuo hiki cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, aliwaita wahanga wa msala huu na kuwasamehe, tena kwa msamaa usio na barua.

Inachanganya kuona kwamba mtu umemfukuza kwa barua na unamrudisha kwa kutompa barua, hii haina matatizo ya kisheriakweli au ndo mtindo wa mazoea kwamba mimi ndo kila kitu na ninachosema ndicho kifanywe hata kama kuna bodi yenye dhamana ya chuo hiki

Sunday, May 14, 2006

NIRIPOTI KWA NANI!!!!

Inashangaza sana kama unahubiri kitu bila kuwashirikisha unaowahubiria.

Hivi nikitoka likizo ninaripoti kwa nani au ni kutafuta visa tu. Nitaandika tena kuhusiana na hili kwani kuna mwanafunzi amerudishwa nyumbani kisa amechelewa kuripoti na mbaya zaidi huu ni mwaka wake wa mwisho. Tuelezwe tulipoti kwa nani au kuna kingine nyuma ya pazia

Saturday, May 06, 2006

UMEISOMA HABARI HII!!!!!

Imetoka katika gazeti la Mtanzania April1 eti kuwa kaimu msajili wa chuo cha MNMA amemkaba na kumpora mwanachuo. Hii si habari njem a kwa chuo chenye jina la muasisi wa Tanzania na kama haina ukweli basi ni vizuri tukapewa ukweli halisi ili kuondoa mawazo na maneno yanayoibuka bila mpango. UPOOOOOOO!
UMEISOMA HABARI HII!!!!!

Imetoka katika gazeti la Mtanzania April1 eti kuwa kaimu msajili wa chuo cha MNMA amemkaba na kumpora mwanachuo. Hii si habari njem a kwa chuo chenye jina la muasisi wa Tanzania na kama haina ukweli basi ni vizuri tukapewa ukweli halisi ili kuondoa mawazo na maneno yanayoibuka bila mpango. UPOOOOOOO!
KOMPYUTA NDANI YA MILANGO YA CHUMA!!!!!!

Ndugu msomaji nimeamua kuipandisha kurasa hii ambayo niliiandika mwaka jana wakati chuo hiki kikiwa hakina huduma acha ya kompyuta kwa wanafunzi bali hata mtandao kwa ajili ya kuwasaidia katika kutafuta 'material' kulingana na kozi wanazosoma.

Hali sasa ni tofauti kwani milango ya chuma sasa imefunguliwa na kompyuta zipo huku wasimamizi wa maktaba wakiwepo kusaidia wale wote wanaotatizwa na teknolojia hii. Haya ni mabadiliko na tunajua kuna mengi yanakuja. hebu soma nilichoandika kipindi hicho ambacho leo ni historia


Ukifika na kuuliza ni hakika utaambiwa wanachuo wanasoma kompyuta kwani ni kweli kabisa kuna madarasa mawili yaliyojaa kompyuta na bahati nzuri nyingine zimeunganishwa katika intanet. Majibu utakayopewa ukaridhika na upande mmoja basi ukweli halisi huwezi kuupata na utaondoka ukiwa na furaha ya kwamba kweli chuo kimebeba jina linalostahili hivyo nacho kinastahili.

Labda nikuonyeshe upande wa pili wa majibu uatakayoyapata kutoka kwa walengwa wenyewe, wanachuo. Hakuna mafunzo ya komyuta na hakuna mwanachuo anayeruhusiwa wacha kuzigusa kompyuta zenyewe bali hata kusogelea karibu a milango miwili ni shida, milango yote inalindwa na mageti ya chuma na kufuli maalum yaani kama za benki.

Inashangaza sana kwa chuo kama hiki kutowaruhusu wanafunzi kutumia vifaa hivi kwa ajili yua kujisomea na kufanya kazi nyingine za kitaaluma kwani hakuna ubishi kwamba intaneti inamwezesha msomaji kusoma vitabu vingi na vya wakati huu.

Juzi nimekutana na rafiki yangu namfahamu tangu tukiwa A-level, yupo hapa chuoni na alikuwa library akitafuta kitabu cha Rural Sociology ambacho hakipo katika 'shefu' za maktaba, alisikitika na nikamwona akimjongea mhusika wa library kujaribu kumwomba agoogle' apate japo nini cha kusoma

Hii haipendezi na hasa kama mtu mzima anapohubiri mabadiliko bila kubadilika akitegemea anaowahubiria wabadilike! Inawezekana tu kama wanaohubiriwa wataamua kumbadilisha yeye kwanza na bila kujali watatumia nini kumbadilisha

Nadhani ujumbe huu ni salamu tosha kabisa kwa MASO kutambua kwamba wapo kama daraja la kutusemea sisis tunataka nini, na si kukaa tu wakilipana posho kwa pesa tunazokatwa kama ada ya chama

Pia uongozi hasa kamati ya taaluma ambayo naamini kabisa inaongozwa na mtu anayependa wanafunzi wajifunze vizuri katika mazingira rafiki uatalifikiria jambo
hili