Friday, February 16, 2007

BARABARA YA KATI INAHITAJI MIUJIZA...!!!!!

Wiki jana nilikuwa ndani ya basi toka Dar kuelekea Mwanza kwa ajili ya kukamilisha utafiti wangu kuhusu kuongezeka kwa wapigadebe katika vituo vya mabasi. Chuo kilitoa muda mfupi uliolazimu sisi tunaotoka mikoani kutafuta usafiri wa haraka ili kuwahi kalenda. najua unafikiria ndege, kwangu mimi usafiri wa haraka si ndege, ni basi.

Tuliondoka kwa basi la Mohammed ambalo nalo kama ilivyokuwa kwa barabara ya kati toka dodoma kwenda singida, lilikuwa ni bovu isivyo kawaida kiasi cha kutulazimu kuingia Dodoma saa 4 usiku. hata hivyo hii si ishu yangu ya leo, leo nataka kuongelea ubovu wa barabara hii maarufu kama njia ya kati.

Barabara hii ni mbovu sana na hasa katika kipindi hiki cha mvua, maeneo ya manyoni na baadhi ya vipande vya tinde hali ni mbovu sana.
Hali hii inashangaza sana kwani serikali kuanzia ile ya awamu ya tatu ilikuwa ikihubiri kwamba ni mapema tu mtu ataweza kutoka mwanza mpaka mtwara kwa gari dogo 'tax'.

Kandarasi aliyepewa kufanya shughuli ya kujenga barabara hii angekuwa ni mtanzania basi tungesema ni ndugu wa kigogo lakini kwa kuwa ni mgeni basi hapo kwa akili ya kawaida kabisa tuliyozoea sis basi tunasema kuna mtu kala, kwani huwezi kumpa mkandarasi asiye na uwezo kazi kubwa kama hii.

Nitakuandikia tena kuhusu tatizo la usafiri ambalo kwa kuwa viongozi wanatumia usafiri wa haraka,ndege, kwao si tatizo

Thursday, February 01, 2007

KUKOSEKANA KWA HUDUMA ZA KOMPYUTA CHUONI KUNA SABABISHA USUMBUFU KWA WANAFUNZI......

Unashangaa kuona kichwa hicho, najua unategemea kabisa hili kutokuwa tatizo katika chuo tena cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere. Umekosea.

wakati shule zinazoitwa za 'academy' (sio academy ya mwalimu nyerere) siku hizi watoto wanafundishwa kompyuta, hali hii ni tatizo hapa chuoni kwani ukitaka kufahamu ni wanachuo wangapi wana uwezo wa kutumia kompyuta basi idadi yao itakusikitisha na kukufanya labda ufikiri kuwa hapa kumejaa ubabaishaji tu.

Sio kwamba kompyuta hakuna, la, zipo kama 40 lakini zima ndani ya vyumba vyenye milango ya chuma na mlinzi nje kuhakikisha kuwa hakuna anayechungulia na kuona vitu vya ajabu, kompyuta.

Mkuu kateuliwa na labda tunaweza kuanza kuiona kompyuta 'live'

Tungoje na kwa wale wasiojua basi wasubiri au waende wakajiandikishe katika akademia za kitoto
KAULA TENA!!!

Kila mmoja alikuwa na mshawasha wa kutaka kujua ni nani atashika nafasi ya ukuu wa chuo cha kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, wengi walikuwa wakifikiria mabadiliko......

Majuzi waziri wa elimu ya juu kafanya kile ambacho alipaswa akifanye, kuteua mkuu wa chuo nafasi ambayo ilikuwa inashikiliwa na daktari Magotti ambaye pia ni kada mkubwa chama tawala CCM.

Uteuzi umefanyika na aliyeteuliwa kuwa mkuu wa chuo ni yuleyule aliyekuwa akikaimu na ambaye amekuwa mkuu wa chuo tangu kilipokuwa chuo cha chama na sasa chini ya serikali.

Ndiyo, jina jipya la chuo lakini mkuu yuleyule, hii ina maanisha kuwa tutegemee mengi na makubwa toka kwa kiongozi mkongwe.

machweo inamtakia dr Magotti kazi njema na itampa ushirikiano wa kutosha kama tulivyoombwa na msarifu ambaye naye ana kaimu nafasi hii, kwa maoni yetu sisi wana machweo tunadhani hata msarifu arudishwe yuleyule na pia korando likarabatiwe liwe jipya.