Friday, February 16, 2007

BARABARA YA KATI INAHITAJI MIUJIZA...!!!!!

Wiki jana nilikuwa ndani ya basi toka Dar kuelekea Mwanza kwa ajili ya kukamilisha utafiti wangu kuhusu kuongezeka kwa wapigadebe katika vituo vya mabasi. Chuo kilitoa muda mfupi uliolazimu sisi tunaotoka mikoani kutafuta usafiri wa haraka ili kuwahi kalenda. najua unafikiria ndege, kwangu mimi usafiri wa haraka si ndege, ni basi.

Tuliondoka kwa basi la Mohammed ambalo nalo kama ilivyokuwa kwa barabara ya kati toka dodoma kwenda singida, lilikuwa ni bovu isivyo kawaida kiasi cha kutulazimu kuingia Dodoma saa 4 usiku. hata hivyo hii si ishu yangu ya leo, leo nataka kuongelea ubovu wa barabara hii maarufu kama njia ya kati.

Barabara hii ni mbovu sana na hasa katika kipindi hiki cha mvua, maeneo ya manyoni na baadhi ya vipande vya tinde hali ni mbovu sana.
Hali hii inashangaza sana kwani serikali kuanzia ile ya awamu ya tatu ilikuwa ikihubiri kwamba ni mapema tu mtu ataweza kutoka mwanza mpaka mtwara kwa gari dogo 'tax'.

Kandarasi aliyepewa kufanya shughuli ya kujenga barabara hii angekuwa ni mtanzania basi tungesema ni ndugu wa kigogo lakini kwa kuwa ni mgeni basi hapo kwa akili ya kawaida kabisa tuliyozoea sis basi tunasema kuna mtu kala, kwani huwezi kumpa mkandarasi asiye na uwezo kazi kubwa kama hii.

Nitakuandikia tena kuhusu tatizo la usafiri ambalo kwa kuwa viongozi wanatumia usafiri wa haraka,ndege, kwao si tatizo

No comments: