Tuesday, June 19, 2007

SAFARI YA GHANA INAKUJA!!!!

Hata sisi tunaweza. Ndivyo ninavyoweza kusema baada ya timu yetu ya soka inayofundishwa na Maxio Maximo kuifunga timu ngumu ya Bukinabe kwa goli 1-0 katika uwanja wa ugenini (burkinafaso).

Kwa sasa timu yetu si kichwa cha mwendawazimu kama ilivyokuwa imezoeleka hapo mwanzo. Tunaweza. Vijana wamefanya mabo makubwa ambayo kila mtanzania anayapenda. Tumepewa raha na hakuna wa kutuzuia sasa, mwendo mdundo.

Pamoja na hayo napenda kuwasikitikia baadhi ya wachezaji ambao walijiona wao ndo wao na wakawa wanaleta nyodo, sasa wanasaga meno kwani vijana wadogo wanafanya mabo amabyo wote tunayataka.

Nafurahishwa sana na msimamo wa kocha wa kutokubembeleza, huu ni mfano mzuri kwa walimu wazalendo. Tunaweza.

Unamkumbuka Kaseja pamoja na Mgosi walivyotoa maneno ya kipuuzi? yako wapi, Tunaweza bila wao kwani wapo wachezaji kibao vijana na wenye nidhamu ambao wanawajibika kwa taifa si kwa friend s of nini sijui., pumbavu. Kwa sasa wenzao wanapeta tu na jana wamepata shavu bungeni ambako kila mtu anatamani walau aingie. Cheki zawadi walizopata!

Waziri mkuu kawaahidi mambo makubwa sana endapo wataenda Ghana, na nyumba nazo hizo zinakuja yaani kutakuwa na mtaa wa Maksimo. Kitakuwa ni kijiji cha utalii, nami nitatembelea na kupiga picha.

Tunaweza
SAFARI YA GHANA INAKUJA!!!!

Hata sisi tunaweza. Ndivyo ninavyoweza kusema baada ya timu yetu ya soka inayofundishwa na Maxio Maximo kuifunga timu ngumu ya Bukinabe kwa goli 1-0 katika uwanja wa ugenini (burkinafaso).

Kwa sasa timu yetu si kichwa cha mwendawazimu kama ilivyokuwa imezoeleka hapo mwanzo. Tunaweza. Vijana wamefanya mabo makubwa ambayo kila mtanzania anayapenda. Tumepewa raha na hakuna wa kutuzuia sasa, mwendo mdundo.

Pamoja na hayo napenda kuwasikitikia baadhi ya wachezaji ambao walijiona wao ndo wao na wakawa wanaleta nyodo, sasa wanasaga meno kwani vijana wadogo wanafanya mabo amabyo wote tunayataka.

Nafurahishwa sana na msimamo wa kocha wa kutokubembeleza, huu ni mfano mzuri kwa walimu wazalendo. Tunaweza.

Unamkumbuka Kaseja pamoja na Mgosi walivyotoa maneno ya kipuuzi? yako wapi, Tunaweza bila wao kwani wapo wachezaji kibao vijana na wenye nidhamu ambao wanawajibika kwa taifa si kwa friend s of nini sijui., pumbavu. Kwa sasa wenzao wanapeta tu na jana wamepata shavu bungeni ambako kila mtu anatamani walau aingie. Cheki zawadi walizopata!

Waziri mkuu kawaahidi mambo makubwa sana endapo wataenda Ghana, na nyumba nazo hizo zinakuja yaani kutakuwa na mtaa wa Maksimo. Kitakuwa ni kijiji cha utalii, nami nitatembelea na kupiga picha.

Tunaweza

Saturday, June 16, 2007

NIPO NDANI YA NYUMBA

Wasomaji wangu kwanza kabisa ningependa kuwaomba samahani kwa kupotea ghafla, nilibanwa na masomo na mitihani ilikuwa inakuja wanguwangu. Sio neno kwa sasa nipo mapumziko na najua tutakuwa pamoja katika kujadili mambo ya utamaduni, siasa na uchumi bila kujali yale yote yanayojiri na kuhusisha maisha yetu