Tuesday, April 18, 2006

MAMBO TAYARI USIKU MSIUWEKE!!!
Ni matumaini yangu kuwa mmekuwa na mapumziko mazuri kwa kila mmoja, nami nimekuwa na mapumziko swaafi kabisa na kuweza kuwasiliana nndugu na marafiki kama unavyojua tena mapumziko yakiisha unapaswa uwe kambini ili kufanya kile chuo,jamii na wewe mwenyewe unachotarajiwa kufanya.
Naam, mambo yamekwisha anza na mapema tu kipyenga kikapulizwa 18/04 na kama kawaida malekchara wakaanza kumwaga lekcha! Unashangaa kuna darasa lilikuwa mahudhurio ya wanafunzi 5, hii haijakaa mwake jamani msiuweke kwani imeshatangazwa kwamba siku ya kufungua na masomo kama kawa.
Wahi usiuweke, duh! inaonekana nyasi zilizozunguka mazingira ya chuo zinapenda sana mvua kwani zilivyoota uatashangaa na laiti kama makwanja yangekuwa yanafanya kazi basi zingeweza kufyekwa kwa ustadi ili kuzifanya zivutie zaidi, nadhani kila mtu analiona

Monday, April 17, 2006

DALADALA NA WANAFUNZI!!!!

Kama kuna mji ambao wanafunzi wanakuwa na wakati mgumu wa kwenda na kutoka shuleni ni Dar. Hii ni kwa sababu namba kubwa ya wanafunzi hawa wanasoma shule za kutwa zilizo mbali hivyo kuwafanya wategemee usafiri wa daladala kwani serikali ya Dar haitoi maelezo ya kutosha kuhusu mradi wa magari ya wanafunzi.
Juzi nimepanda daladala na nikashuhudia sheshe zito kati ya kondakta na 'dent' Hakuna aliyetaka kushindwa kila mmoja alikuwa ni mbabe kwa mwenzake konda anataka nauli ya mtu mzima na denti anatoa 50/=na kitambulisho cha shule anayosoma. Tafrani inaishia kwa abiria kuwa upande wa dent na kila kitu kikawa kama kawaida.
Inanikumbusha wakati ninasoma sekondari na siku moja nikampa konda50/= na kitambulisho cha shule niliyosoma Ndanda (Naleo Pasona en grata, Mwaimu, Limbu, na wengi najua mnaikumbuka shule hii) kumpa kitambulisho akashangaa na kuniuliza kama Ndanda Kosovo ( mwanamuziki wa wajelajela) kama ana shule. Sikutaka kumjibu kwani ni mazoea kwa konda na denti kila mtu kumtegea mwenzake nani aanze kutoa kashfa inayofuatiwa na vita kali ya maneno baini ya wawili.
Bahati nzuri mzee mmoja wa makamo akamshangaa konda kwa kutofahamu hata shule ambayo rais mstaafu Ben Mkapa aka Mr Clean alisoma, konda ulimi ukakatwa nami nikatulia kwa kujiamiani kituo kilichofuata nikashuka.
Nadhani ni wakati muafaka kwa wanadar kujadili ni kwa vipi tatizo la usafiri wa wanafunzi linaweza kutatuliwa pia na mikoa mingine, kila mmoja ashiriki bila kujali ni nani na ana nini!
Jumatatu njema ya pasaka

Saturday, April 15, 2006

ILIKUWA NI TERM YA FURAHA!!!

Wow! Kwa mara ya kwanza!

Barua ya Kaimu Mkuu wa Chuo cha MNMA ilibandikwa ubaoni ikitoa 'shavu' kwa Mr O. K. Temwende ( Kaimu Naibu wa Mkuu wa MNMA) na kamati yake ya taaluma kwa kufanikisha utaratibu wa chuo kuanza kutoa B.A. Mara zote tunajua wakubwa hupongezana ndani kwa ndani na wakati mwingine mkubwa sana hampongezi mdogo na hatambui mchango wake lakini kwa mara ya kwanza barua ya Dk Magotti inasomwa na kila mtu na wote tunakubali na kuithamini kazi ya Mr Temwende. Bravo Mr Temwende na kamati yako!

Wanachuo wote tunapewa vitambulisho vizuri kabisa ( sina uhakika na ubora wake hususani ile nailoni kuachia na kufanya karatasi kuchanika! nakumbuka jinsi dean of student alivyochachalika kuhakikisha vijana wake tunatembea tukiwa tunatambulika,( unamkumbuka yule jamaa wa SS1 aliyesema kwamba alikamatwa na polisi kitambulisho cha kuazimia vitabu maktaba kikamuokoa! Alikuwa anatoka kuwachangia tbl kuwafanya watoe kodi kubwa kwa serikali na mishahara minono kwa wafanyakazi wakitukutanisha pamoja bushtrekker tehetehete!

Hivi tangazokwamba kuna mafunzo ya kompyuta linatuhusu wote

Saturday, April 08, 2006

SIKUKUU NJEMA!!!


Najua kila mtu anajiandaa kwa ajili ya sikukuu mbili kubwa kwa watu wa madhehebu yote makubwa ya dini za kigeni, Waislamu na Wakristo

Najua kabisa kwamba waislamu mtakuwa na maulid ya Mtume na baadaye Wakristo watafungua kwarezima na hivyo kusheherekea Pasaka

Machweo inawatakia sikukuu njema na mkae mkijua kwamba jumatatu chuo kinafunguliwa na usishangae jumanne kukawa na paper si unajua mambo ya kasi mpya na kwa mara ya kwanza
Peace&Love from Geka
HII HAIJATULIA WAZEE

Sina hakika na mitihani tuliyofanya kama ilikuwa imeandaliwa kwa umakini wa kina na kwa kuzingatia hali halisi na jina la chuo.

Usishangae kwani kwa sasa kila kiti kiko wazi kwani sheria ya nchi inatamka wazi bila kigugumizi kuwa sasa hakuna chuo kinachoitwa Kivukoni Academy of Social Science (KASS). Cha ajabu kabisa ambacho kwa sababu tu ya mazoea ya watu kushindwa kuhoji ni kwamba mitihani tuliyofanya ratiba ilikuwa inaonyesha kuwa wanaofanya ni wanachuo wa KASS na si wa MNMA.

Ukiachana na ratiba bado karatasi za kujibia zilikuwa na mihuri ya KASS na si MNMA kama inavyotakiwa kuwa kwani shughuli zote za KASS zimerithiwa na MNMA.
Hii inachanganya na wakati mwingine mtu yeyote bila nia ya kutaka kumsema mtu utaona kwamba ni kama uandaaji wa ratiba na upigaji mihuri ulikuwa ni wa kushangaza kwani mitihani imeandikwa MNMA ratiba na karatasi za kufanyia mitihani zinaandikwa KASS, labda inawezekana kabisa kwamba haya matangazo ni danganya toto na MNMA haijarithi chochote toka KASS

Ninakaribisha maoni kama unaweza kuchangia kwa hili bila kumkashifu na kumsingizia mtu.
Najua wengi sasa mtakuwa na hamu ya kujua nini kinaendelea katika chuo hiki kisicho na journal wala gazeti. Tumia blog hii kusema nini unafikiri na toa mawazo yako ya kitaaluma ili kusaidia wanachuo wote kwani chuo ni zaidi ya majengo na wanafunzi