Saturday, April 08, 2006

HII HAIJATULIA WAZEE

Sina hakika na mitihani tuliyofanya kama ilikuwa imeandaliwa kwa umakini wa kina na kwa kuzingatia hali halisi na jina la chuo.

Usishangae kwani kwa sasa kila kiti kiko wazi kwani sheria ya nchi inatamka wazi bila kigugumizi kuwa sasa hakuna chuo kinachoitwa Kivukoni Academy of Social Science (KASS). Cha ajabu kabisa ambacho kwa sababu tu ya mazoea ya watu kushindwa kuhoji ni kwamba mitihani tuliyofanya ratiba ilikuwa inaonyesha kuwa wanaofanya ni wanachuo wa KASS na si wa MNMA.

Ukiachana na ratiba bado karatasi za kujibia zilikuwa na mihuri ya KASS na si MNMA kama inavyotakiwa kuwa kwani shughuli zote za KASS zimerithiwa na MNMA.
Hii inachanganya na wakati mwingine mtu yeyote bila nia ya kutaka kumsema mtu utaona kwamba ni kama uandaaji wa ratiba na upigaji mihuri ulikuwa ni wa kushangaza kwani mitihani imeandikwa MNMA ratiba na karatasi za kufanyia mitihani zinaandikwa KASS, labda inawezekana kabisa kwamba haya matangazo ni danganya toto na MNMA haijarithi chochote toka KASS

Ninakaribisha maoni kama unaweza kuchangia kwa hili bila kumkashifu na kumsingizia mtu.
Najua wengi sasa mtakuwa na hamu ya kujua nini kinaendelea katika chuo hiki kisicho na journal wala gazeti. Tumia blog hii kusema nini unafikiri na toa mawazo yako ya kitaaluma ili kusaidia wanachuo wote kwani chuo ni zaidi ya majengo na wanafunzi

1 comment:

Anonymous said...

Hiyo haikuwa imetulia kabisa.Ni jambo la aibu sana kwamba vyuo vingi vinakuwa vinafanya kazi zao kama vile haviongozwi na wasomi.