Monday, February 13, 2006

KASSO HII NI AIBU

Huwezi kutegemea kitu hiki kitokee katika taasisi ya elimu ya juu kama hapa The Mwl. Nyerere Memorial Academy, imetokea

Inashindikana nini kwa matangazo yanayowahusu wanachuo kuandikwa kwa kompyuta, katibu mzima wa kasso anaandika tangazo na linabandikwa notice board likiwa na maandishi ya mkono na bado huyuhuyu unamtegemea aingie karne ya 21
jirekebishe
KARIBU THE MWALIMU NYERERE MEMORIAL ACADEMY

Hii sio zile Academy zinazoibuka hapa nchini kama uyoga kwa kuwa tu zinawafundisha watoto kiingereza, Ni ACADEMY kwa maana yake.
Siku za nyuma nilikuhadithia kidogo kuhusu kubadilika kwa jina kwa chuo cha Syansi jamii kivukoni, naam sasa kwa sheria rasmi namba 6 iliyopitishwa na bunge na kutiwa sahihi na rais wa jamhuri ya Tanzania imeruhusu kuanzishwa kwa chuo cha kumbukumbu ya Mwl Nyerere.
Kuna mengi ya kukueleza lakini tulia na nitakuwa nikikupa vyote unavyotaka kujua kuhusu chuo hiki kinachotoa shahada, stashahada na astashahada katika sayansi jamii na uchumi/maendeleo
MAHITA ANAPOKUWA MWANASIASA

Huku akiwa ameshika visu vipya vikali vya jikoni, IGP huyu anatoa siri ya kwamba ni jinsi gani alivyokuwa mwiba mkali kwa wanaCUF na kuwafanya wasipate ushindi katika uchaguzi ulioiweka CCM madarakani.
Kamanda nandai kwamba Chama cha Wananchi ndicho kinahusika na mipango ya ujambazi unaotokea katika mabenki hapa Dar. Kwa wasiojua ni kwamba wimbi la ujambazi limetokea katika mabank kadhaa hapa Dar huku mamilioni ya shilingi yakiporwa mchana kweupe na watu wenye silaha, sio visu vya kukatia vitunguu Mahita anavyotaka kutuaminisha kuwa wenye visu hivyo (CUF) wanahusika na uporaji huu.
Hakuna benk/maduka ya fedha na vito hata moja ambapo majambazi yamengia na visu katika kutekeleza majukumu yao. Yanaingia na bunduki kubwa kubwa na si visu kwani hayaendi kuiba vitunguu au kukata kachumbari hivyo kutuonyesha visu na kujisifu kuwa umewazuia CUF kupata ushindi unakuondolea sifa zote za kuwa IGP wa Tanzania, bora ufanye kazi ya siasa na si kutumia ofisi ya watanzania kwa manufaa yako
Pumzika ule pensheni yako waachie Mapolisi wafanye kazi kwa masilahi ya Watanzania na wala si kwa malslahi ya CCM, CUF au CHADEMA