Monday, March 27, 2006

TUKO MAPUMZIKO


YaaaH! Baada ya mitihani kwisha sasa tuko katika mapumziko ya kama wiki tatu. Ningependa sana nikusimulie kuhusu yale yote yaliyojiri katika kipindi cha examz, nakuahidi nitafanya hivyo kwa sas relax

Sunday, March 19, 2006

Wow! Nmerudi tena. Baada ya kimya kifupi, sasa ninakuja tena na kitu kipya na cha kawaida kabisa kwenye higher institution kama hii ya kwetu. Wiki kesho tunaanza mitihani ya kwa ajili ya term ya pili kwa mwakahuu. Ninachukia mitihani lakini ndo hivyo tena kwani hakuna maana ya kusoma kama hujaribiwi kwa kile ulichokisoma.
Nawajua wengi amabo kila wakisikia mitihani baaasi kuumwa si kuumwa na kila kitu kinabadilika yaani wanaweza kusahau hata kuoga.
Ninachukia mitihani lakini si kama ninaiogopa, la , siwezi kuiogopa kwangu mtihani mgumu kabisa ulikuwa ni wa darasa la nne ambapo kila mwanafunzi kipindi kile alikuwa na kitete cha kuingia darasa la tano. Siidharau mitihani hii ila ni kwamba ninataka kuwaencourage watahiniwa wenzangu kwamba kama wao waliomaliza walifaulu kwa nini sisi tushindwe,
Nawatakia mitihani mizuri na mfanye mkiwa na moyo wa kijiamini. Love

Thursday, March 09, 2006

MWANA 'MASO' BLOGU HII NDILO GAZETI LAKO, LITUMIE




Ni jambo la kushangaza kwamba jumuia ya chuo hiki kilichobeba jina la baba wa taifa la Tanzania Mwl. J. K. Nyerere hakina gazeti la wanachuo. Kila mwenye mawazo yake timamu atajiuliza na kupata jibu lazima awatafute wahusika, nimewatafuta na jibu kutoka kasso halieleweki

Si kwamba hawajui maaana ya gazeti kwa wanachuo la, ni uzembe na mazoea ya labda kwa kuwa library kuna Mtanzania na Rai, Daily Newz na hivi wanachuo wanapaswa wasome na si kuchangia hoja zao katika gazeti lao.

Kwa kuona tatizo hili ninakuomba mwanachuo mwenzangu tumia blogu hii kutoa maoni yako ya aina yoyote ilmradi tu haumtukani yeyote. Tumia lugha yoyote ila ningependa sana kama ukatumia Kiswahili ili na wengine wengi wanaojua maana ya lugha hii katika kuwasiliana wakasoma na kufurahi, kuongeza uelewa na kushiriki katika mijadala mbalimbali ninayoitegemea kutoka kwako.

Nina imani kabisa hata serikali ya wanachuo itakuwa na nafasi ya kuchangia na kueleza yote yanayojitokeza ofisini kwao. Najua matangazo yao mengi wanayatoa kwa kuandikwa kwa mkono lakini kwa kuwa chuo kitaendesha kozi ya kompyuta basi natumaini hali itabadilika na pale ubaoni hatutaona tena tangazo lililoandikwa kwa mkono toka Administration na katika serikali ya wanachuo.

nakukaribisha sana katika blogu hii jisikie huru kutoa mawazo yako yenye kujenga jamii nzima si ya wanachuo tu bali ya wasomaji wote wa ndani na nje ya nchi kwani ni ukweli kwamba blogu haina mipaka na kazi ya kuihariri inahitaji busara ya kutembea na taa mchana
KIKAO CHA SERIKALI YA WANACHUO


Kwa mara ya kwanza tangu nijisajili kama mwanachuo wa hapa THE MNMA juzi tumekaa kikao cha kwanza huku mkuu wa Principal akiwa mgeni rasmi na katika hali ya kushangaza kabisa Dean of Student akawa ndio kama 'MC'wa kikao hicho.

Nilitegemea lugha itakayotumiwa itakuwa ni ya kistaarabu na kirafiki hasa kwa kikao kama hiki cha watu wenye akili zao wanaohitaji kuelezwa yote yanayoona sawa si sawa kwao.

Nitajitahidi kukuletea yote yaliyojiri katika ukumbi huu wa bush trekker

Muhimu ni kwamba kumbuka kwamba ada inatarajiwa kuongezwa kwa kuwa tu kutakuwa na masomo ya kompyuta