Saturday, September 30, 2006

KUMBE WATANZANIA TUNATUMIKISHA WATOTO!!!

Baada ya Sauper kutuonyesha jinsi tunavyokula samaki mabaki, rais alipiga sana kelele na kuungwa mkono na kila mtu ambaye kwake Darwin9tmare ilikuwa ni uongo kwa kuwa tu kasema raia namba moja.

Sasa kuna hii filam ya IRIN inayoitwa GEM SLAVES Tanzania's Child Labour yaani kwa kiswahili rahisi "utumikishwaji wa watoto katika migodi" filam hii imechukuliwa huko Mirerani wakionyeshwa wanaapollo na 'nyoka' wakifanya kazi ngumu za kutafuta tanzanite wasiyofaidika nayo.

Tumezoea kuandamana na sasa tuusubiri wakazi wa A-town waende barabarani kuilaani filam hii. na cha mno tusubiri rais atakapoenda kuongea na wazee wa arusha atasema nini, kwa kuwa atakachosema kitakuwa ni sahihi kwa watu wanaofikiri kwamba atakalosema ndilo sahii basi tujiandae kuunga mkono hata kama hatujaiona filam yenyewe kama ilivyokuwa kwa wale 'wazalendo' wa mwanza walioandamana kumpinga Sauper bila kuiona hata 'mapanki' yenyewe
NIKO LIKIZO


Nadhani ni kipindi kimepita tangu niweke kitu kipya gazetini. Wengi pia mmekuwa mkiniuliza kwa sms tatizo nini mbona sionekani tena gazetini au ndo kuchoka kwa kazi ngumu ya kuandika. NO. Niko likizo na maeneo niliyopo mtandao ni tatizo na hata ukipata nafasi katika intanet gharama wanazotoza ni kubwa ukizingatia mtoa huduma yupo peke yake 'monopoly'. kwa sasa nimepata nafasi hii kwani niko jijini kwa shughuli maalum.

Wasomaji wangu kaeni mkitambua kuwa nipo na blog hii haiwezi kuwaacha peke yenu