Thursday, October 18, 2007

MAADHIMISHO YA KIFO CHA NYERERE

Juzi chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere kimeungana na watanzania wote kuadhimisha miaka nane tangu kufariki kwa kiongozi wa kwanza wa taifa hili, Mwalimu Julius Nyerere. Sherehe zilikuwa nzuri na zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama na serikali akiwamo wazri Kingunge Ngomale Mwiru aliyekuwa mgeni maalum hapa chuoni.

Yaliongewa mengi na tukaoneshwa mengi kuhusu malimu, hakuna aliyepingana nayo. Mada mbalimbali zilizoandaliwa na wahadhiri na wanafunzi zilitolewa katika maadhimisho haya yaliyofanyika kwa siku mbili. Wachangiaji mbalimbali walichangia hii yote ikiwa ni katika kuonesha kuwa kila mmoja anamtambua na kumthamini mwalimu.

Tatizo langu linakuja pale tu wale tuliowategemea kumwonesha mwalimu kama kiongozi wa watanzania wanamwonyesha kama kiongozi wa CCM. Kingunge pamoja na dhamana aliyokuja nayo ya mtumishi wa umma alishindwa kujizuia kutamba kuwa mwalimu ni wa CCM pekee na wanasiasa wanaomwiga wanafanya makosa kwani wao si wanasisisemu.

Kikubwa pia kilichonitatiza ni pale iliposemwa kuwa mwalimu alijali mali na wananchi, hapa naona ni kama tunadanganyana mchana kabisa, ni kweli kwamba mwalimu alijali wanacnhi kwa kutogawa maliasili za nchi.

Wale wanaojidai kuwa mwalimu ni wao leo tunawaona wakiongoza kwa kuuza nchi na utajiri wake, tazama mikataba mibovu inavyosainiwa kila kukicha na pia angalia jinsi mwananchi wa kawaida anavyotaabika kwa bidhaa kuwa ghali huku viongozi na watoto wao wanavyotanua kutokana na kuendekeza matumbo kuliko watu.

Si busara kumuenzi mwalimu kwa kuimba nyimbo zake huku mkicheza ngoma za ubinafsi, ufisadi na mabaya mengine mengi ambayo ni mwiba kwa watanzania, sanamu tu hazitoshi kuonesha kuwa tunamjali mwalimu bali tukumbuke kuwa mwalimu aliona na kuheshimu mali za watanzania na hakutaka kuzitumia kwa manufaa yake binafsi
HE! ETI KISWAHILI SIO LUGHA YA WASOMI!!!??


Kama kuna siku niliyoshangaa basi ni siku ya Alhamisi, tukiwa katika mjadala hapa darasani, nilizuiwa kuchangia mada kwa kuwa tu nilipaswa kuongea kiingereza. Nilikumbushwa kuwa lugha rasmi ya mawasiliano katika vyuo vya elimu ya juu ni kizungu na eti Kiswahili ambacho ni lugha ya taifa huru la Tanzania hakina nafasi kwa wasomi wasiosoma lugha hii kama somo.

Wengi walishangaa, niliamua kukaa na mwenyekiti alinionya kutoongea lugha hii tena, na hasa ninapokuwa darasani. Mwisho sana mhadhiri wa somo alisimama na kuniruhusu kuchangia mawazo yangu katika mada iliyowasilishwa na kundi la pili iliyohusu 'ulinganifu kati mitizamo ya kisiasa mmoja ukiwa ni mtazamo kongwe na mtazamo wa kisasa'

Kikubwa ninachopaswa kuwauliza ninyi wengine ni hiki, Je Kiswahili si lugha ya mawasiliano katika sehemu za elimu ya juu? au ndo nimuamini yule mzazi kule kwetu anayajua kwamba kama huwezi kuongea kizungu wewe si msomi, tena nikakumbushwa tu kuwa Kiswahili si chochote na halafu tunapaswa tujifunze Kichina
NIMERUDI TENA!!!

Mpendwa msomaji wa blogu hii, kwanza naomba uniwie radhi sana kwa kuwa kimya kwa kipindi kirefu. Nilikuwa nimebanwa na majukumu mazito ya masomo, nafurahi kwamba wanajumuia wenzangu wanaoblogu kwa Kiswahili walifanya kile ambacho wote tunahitaji, habari, taarifa, na burudani.

Kubwa zaidi kwa sasa ni kuendeleza kile wenzangu walichonacho na kama unavyojua jukumu la ukurasa huu ni kukuhabarisha na kusikia wewe unasema nini kuhusu mada mbalimbali ambazo ama ntakuwa nimezichokoza ama wewe ndo umeanzisha.

Natambua kabisa yapo mengi sana ya kujadili ambayo magazeti yetu hayana nguvu ya kuvijadili. Kuwepo kwako kutasaidia wengine kufahamu mengi na kuelemika na hivyo kujitambua.

KARIBU SANA