Thursday, October 18, 2007

NIMERUDI TENA!!!

Mpendwa msomaji wa blogu hii, kwanza naomba uniwie radhi sana kwa kuwa kimya kwa kipindi kirefu. Nilikuwa nimebanwa na majukumu mazito ya masomo, nafurahi kwamba wanajumuia wenzangu wanaoblogu kwa Kiswahili walifanya kile ambacho wote tunahitaji, habari, taarifa, na burudani.

Kubwa zaidi kwa sasa ni kuendeleza kile wenzangu walichonacho na kama unavyojua jukumu la ukurasa huu ni kukuhabarisha na kusikia wewe unasema nini kuhusu mada mbalimbali ambazo ama ntakuwa nimezichokoza ama wewe ndo umeanzisha.

Natambua kabisa yapo mengi sana ya kujadili ambayo magazeti yetu hayana nguvu ya kuvijadili. Kuwepo kwako kutasaidia wengine kufahamu mengi na kuelemika na hivyo kujitambua.

KARIBU SANA

No comments: