Monday, June 23, 2008

MAXIMO ANA MCHANGO MDOGO SANA KATIKA SOKA LA TANZANIA

Najua wapo wanaoamini kuwa ufanisi wa Taifa Starz umechangiwa na kocha wa kibrazil aliyeletwa na JK. Kwangu mimi hali ni tofauti na wote wanaotangaza kuwa Tanzania imetangazwa na Maximo.

Kuna vitu kama viwili ambavyo ndivyo vimeifanya Taifa stars ifikie kiwango hiki ambacho hata hivyo hakijafikia kiwango kilichooneshwa na timu yetu ya taifa kwenye miaka ya 80. Vitu hivi ni kama vifuatavyo:-

Sapoti kubwa ya serikali kwa timu: Hii ndiyo chachu kubwa sana ya timu yetu kufanya vizuri. Wakati mbrazil anakuja si kweli kuwa timu yetu ilikuwa mbovu kiasi cha kusema kwamba alitukuta tuko wodi ya wagonjwa mahututi. serikali miaka ile baada 80 haikuonesha kipaumbele katika kusaidia timu ya taifa. Rais JK alipoingia madarakani kuliendana na mabadiliko makubwa katika utendaji wa TFF (zamani FAT) na hivyo alitambua kiu wa watanzania kuwa ni maendeleo ya soka na hapo ndipo alipoanza kuisadia timu kwa kuipatia kocha na misaada mingine.

Mfumo wa soka letu ulitengemaa na shurani kubwa ziende kwa shule mbalimbali nchini ambazo zilikuwa stari wa mbele kuwapa nafasi vijana wenye vipaji vya soka kujiunga na shule hizo na kuendeleza vipaji vyao, mfano wa shule hizo ni Makongo na Jitegemee kwa DSM. Mikoani napo vijana wenye vipaji walikuwa wanaangaliwa kwa ukaribu zaidi.

Kutokana na muundo mzima wa uongozi wa chama cha soka Tz wadau mbalimbali walijitokeza kuisadia timu ya taifa kwa hali na mali kama tunavyoshuhudia wafadhili mbalimbali ambao wamekuwa wakitoa pesa zao na kudhamini timu ya taifa. Kwa kuwataja kwa uchache hawa ni TBL, Serengeti, NMB na NBC pamoja na makampuni na watu binafsi.

Ukiangalia sababu hizi utagundua kabisa hata walimu wetu wa bongo wangekuwa wakipewa sapoti kama hii wasingeshindwa kuifikisha timu hii hapa ilipo.

Unaweza kufikiria hili na kutoa maoni yako
USISEME UNA MATATIZO

Wadau hii nimeitoa kwa Mzee wa Sumo.

Mzee Kidevu kanitumia hii!Jamaa wawili walikutana kwenye kituo cha basi wakafanya mazungumzo.

Mmoja aling'ang'nia kuzungumzia kero za familia yake hatimaye mwenzake akasema " Unadhani familia yako ina matatizo?"Basi sikiliza kisa hiki.

"Miaka michache iliyopita nilikutana na mwanamke mjane aliyekua na binti mkubwa tu na tukaamua kuoana. Baadaye baba yangu akamuoa binti yangu wa kambo hivyo huyo binti yangu wa kambo akawa mama yangu wa kambo na Baba yangu akawa mtoto wangu wa kambo wa kiume ambapo mke wangu akawa mama mkwe wa mkwe wake.Baadaye binti yamke wangu yaani binti yangu wa kambo alipata mtoto wa kiume. mtoto huyo wa kiume alikua ndugu yangu kwa sababu tulichangia baba mmoja. lakini kwa vile alikua ni mtoto wabinti wa mke wangu papo hapo akawa mjukuu wa mke wangu na mimi nikawa babu yake ndogo wangu.

Lakini hayo yote yalikua si kitu mpaka mimi na mke wangu tulipopata mtoto wa kiume. Sasa msichana ambaye ni ndugu wa mtoto wangu huyo wa kiume kwa kuchangia mama yao mmoja, akawa pia bibi yake. Hali hiyo ilimfanya pia baba yangu kua shemeji wa mtoto wangu ambaye ndugu yake wa kike kwa upande wa mama yao ndie mke wake baba yangu. Kwa hiyo mimi ni shemeji yake mama yangu wa kambo ambapo mke wangu ni mama mdogo (anti) wabinti yake mwenyewe . Mtoto wangu wa kiume ni mpwa wa baba yangu ambapo mimi nikawa babu yangu mwenyewe.

SWALI.Je, unadhani mpaka hapo wewe una matatizo ya kifamilia? Acha kulalamika
HIVI IKIWA NDIVYO, ITAKUWAJE!!!

Hii nimeipata toka kwa rafiki yangu aliyeko Nairobi na ninapenda kuiweka hapa kama ilivyoletwa

Kuna mdau eti laleta hii, jamani kutania viongozi...
Nafurahi kuwajulisheni nyote kwamba kuna vyuo kumi vimefunguliwa maeneo mbalimbali nchini, vikitoa kozi mbalimbali na kubeba majina ya watu maarufu kama ifuatavyo:

* Benjamin Mkapa Institute of Political Entrepreneurship and Openness

* David Balali School of Central Banking and Foreign Debt Management

* Andrew Chenge College of Applied Contractual Law

* Ali Hassan Mwinyi University of Inflation Control

* Karamagi Institute of Mining Licensing and Administration of Mining Contracts

* Zakia Meghji college of Tourism and Protection of Public Funds and Natural Resources

* Ditopile Mzuzuri School of Conveyance and Welfare of Public Drivers

* Mwalimu Nyerere University College of Privatization

* Mkono Intitute of Legal Fraud Prevention

* Lowassa School of Prevention of Fake Companies

Mimi nimefurahishwa na utani huu, sijui wewe