Friday, June 23, 2006

GHANA KATUKOMBOA WAAFRIKA

Wakati mwanablogu mkongwe Ndesanjo Macha wa jikomboe.com analalamika kuwa afika si kitu yaani ni sifuri kwa kila kitu anachokitazama yeye na hasa akatilia maanani eti aibu inayozikuta timu zetu ambazo baadhi zimetolewa katika raundi za makundi

Jana Ghana wamemdhihirishia kuwa afica ndiko mpira unachezwa kwani black star waliwachabanga vijana wa Joji Kichaka kwa mabao mawili kwa moja huku ushujaa ukionekana karibu katika kila sekta ya timu ya Ghana hongera kwa wote na hasa kwa mashabiki tuliojitokeza kwa wingi kuwapa shavu vijana wa Africa.

Tunakutana na Brazil! Tutawashinda na ni bora nikasema kama kiungo mahiri wa Ghana Michel Essien alivyosema "tumecheza nao katika under 17 na 21, tunawajua kwani tuliwafunga bila kusubiri uda wa nyongeza" hakika brazil atapigwa bao 3-1 huku Appiah, na Essien wakifunga na Gyan bao kali la kichwa

SHANGILIA GHANA MABINGWA WAPYA WA KLD

Kwa ushindi huu Afrika imepata nafasi moja ya kuwa na timu ya 6 hapo 2010
NI WAKATI WA MITIHANI

Ukisoma bila kufanya mitihani sidhani kama unastahili kuitwa msomi japo hili linaweza kuwa na maana nyingine ila kwa mtazamo wa machweo mithihani ndicho kipimo sahihi kabisa cha kumtambulisha mwanafunzi na mtu mwingine

Mitihani inaanza j3 hapa MNMA kwa niaba ya wachangiaji na wasomaji wa mada mbalimbali katika machweo ninawatakia mitihani salama wale wote tutakaokaa na kufanya mitihani hii.

Vilevile ni kipindi hiki ndipo tunaagana na wenzetu wanaomaliza mafunzo yao ya diploma na hivyo tunawatakia mafanikio mema huko waendako kutafuta ajira katika dunia hii ya utandawazi

Thursday, June 15, 2006

TUNASUBIRI KUAPISHWA!!!

Hassan Jani ndiye Rais mpya aliyechaguliwa kuiongoza serikali ya MASO-MNMA baada ya kuwashinda wapinzani wake wawili Rama Warioba na Rehema H, katibu wake bado hajapatikana kwani Emmanuel Ndunguru na Janeth Soka walilingana kura na hivyo bado tunasubiri utaratibu mpya wa kumpata katibu mkuu, Viongozi waliochaguliwa ni hawa hapa chini na wanasubiri muda tu waweze kuapishwa ili kuingia kazini na kufanya kazi

Rais;- Hassan Masoud Jani SSI
M/Rais:- Bado
Waziri wa Fedha: Edward Biashara Baridi EDI
Waziri wa Afya: F Katanzi GI I
Waziri wa Ulinzi na Makazi: Adam R. Kikono SSI
Waziri wa Michezo na Mahusiano ya Nje: Samwel Mhinga SSI
Waziri wa Habari: Obeid M. Mashauri SSI
KOMBE LA DUNIA 'KLD'

Kama ilivyo ada kwa watanzania kazi yetu sisi ni kushabikia tu timu za wenzetu. Najua sasa wengi wetu tunajiita Waghana, Angola na wengine tunajiona tuna ukoo na kina kafu! Ronaldo. Hizi tabia ndo zetu na wala hatuna haja ya kujiuliza ni kwanini hatuioni timu yetu ikishiriki katika kombe kubwa kama hili japo mara moja.

Tushiriki ya nini bwana kama watu kombe lilishaletwa tena lile orijinali na tukapiga nalo picha na kisha rais akalibeba kuonesha kwamba sisi si wageni katika suala zima la kabumbu.

najua tumejigawa lakini swali tunalopaswa kujiuliza ni nini tunajifunza kwa kombe hili ukizingatia timu kama Angola inashiriki na kuvitoa jasho vigogo! Tanzania ni nchi ya amani lakini haipendeza kuona ndani ya amani hakuna nafasi ya kujitangaza na sasa soka licha ya kutoa ajira ila ni utalii tosha na nchi kupata wawekezaji katika sekta mbalimbali

Nilitaka kusahau mimi ninashabikia timu hya Ghana na nikiwa kama mchezaji wa soka nafasi ya kiungo mzuiaji na mara mojamoja kufunga ninapendezwa na uchezaji wa Essien, wewe unashabikia timu gani ukiacha Brazil ambayo ni timu ya wote

Furahia michuano mikubwa hii ukijiuliza utafanya nini Tanzania nasi tuweze kushiriki japo raundi ya kwanza

Sunday, June 11, 2006

UCHAGUZI MASO-MNMA UMEKWISHA!!!!!!!!

Mpenzi msomaji wa gazeti hili, juma lililokwisha nilikueleza kuhusu mchakato wa uchaguzi wa serikali ya wanafunzi katika chuo cha kumbukumbu ya mwalimu Nyerere, uchaguzi ulifanyika siku ya ijumaa kuanzia saa kumi jioni na mpaka kufikia saa 12 jioni kazi ya kupiga kura ikawa imemalizika wakasubiriwa mawakala waanze kuhesabu kura 'kula'

nafikiri unajua kuwa nilikuwa ni mmoja wa wagombea nikigombea nafasi ya uwaziri wa habari (usishangae hapa MASO uwaziri unagombea, hawateuliwi yaani wote ni kama maraisi) na nilikuwa na nashindania nafasi hii na mtangazaji wa television Zanzibar.

katika uchaguzi huu nafasi zilizokuwa na ushindani mkali ni nafasi ya urais ambayo ilikuwa na wagombea watatu akiwamo mwanamke mmoja pekee aliyejitokeza ( Anna Senkoro!!!) na vivyo hivyo kwa nafasi ya ukatibu mkuu na makamu wa rais (mtu mmoja anakuwa na cheo chenye nyadhifa mbili).

Upande wa nafasi za mawaziri wizara zilizoshuhudia upinzani mkali ni wizara ya michezo na mahusiano ya nje pamoja na wizara ya afya na kafteria.

Najua unadhani nilishindwa na ndio maaana nazunguka tu bila kukupa matokeo hususani ya wizara niliyogombea.

hakuna kitu kizuri kama kusoma ishara za nyakati na kuzifuata, usipozitii basi yatakayokukuta unaweza ukatafuta wachawi na sababu chekwa huku wapiga kura wakiwa pembeni na tabasamu zito wakikuangalia jinsi unavyohangaika kutafuta chanzo cha wewe kushindwa.

Mpinzani wangu, dada mrembo anayepaka rangi ya shaba nywele zake huku tabasamu tamu likiwa usoni kwake kwa wale anaowafahamu alisoma alama za nyakati na akaona hakika hata angeingia katika mbio hizo basi ingekuwa mashindano ya chui na kobe ambapo mshindi anajulikana.

Siku ya mwisho kabisa alijitoa na nikawa mgombea pekee na ushindi nilioupata siwezi kuuita wa tsunami kwani janga hili linaendana na maafa ila tambua kwamba nilipata ushindi mtamu na ni kura 11tu zilimchagua'mwenzangu' na hizi ni kura mhuhimu kwani zinanifanya nijitambue mimi ni nani na ninapaswa kufanya nini si kwa wale walionichagua tu bali kwa wale muhimu wachache walioamua kutekeleza haki yao ya kidemokrasia kwa kupiga kura kwa mpinzani (niruhusu nmwite kivuli)

Bado tunasubiri nafasi moja kwani wagombea katika nafasi katibu mkuu na makamu wa rais hawakufikisha nusu ya kura ili mshindi aamuliwe na hivyo uchaguzi wao jumanne jioni

Tegemea mazuri katika mchakato huu mapema kwani nitakuletea orodha ya wagombea na kura zao.

tafadhari kumbuka gazeti hili sasa liko chini ya wazir wa Habari-MASO

Saturday, June 03, 2006

ADA JUUUUUUUU!!!!!!

Nilikuandikia wiki jana na kukutaarifu juu ya kupaa kwa ada kwa wanachuo wa MNMA.
Jana Ijumaa kaimu wa mkuu wa chuo akaitisha kikao cha wanafunzi na ajenda kubwa ilikuwa ni kututangazia ada mpya ambayo ni tshs 820,000/= toka laki sita, yaani ongezeko la tshs220,000/=
Shabaaaash!!!!!!

Ongezeko hili ni kutokana na kikao cha bodi kilichoketi na kufanya utafiti wa ada katika vyuo vingine! Vyuo vingine vinavyosemwa kuwa ni adfa kubwa ni vile ambavyo havina mkono wa serikali kwa asilimia mia kama kilivyo vhuo hiki.

Kuna maoni mbalimbali kuhusu ongezeko la ada hii,

Nitakuandikia