Thursday, June 15, 2006

KOMBE LA DUNIA 'KLD'

Kama ilivyo ada kwa watanzania kazi yetu sisi ni kushabikia tu timu za wenzetu. Najua sasa wengi wetu tunajiita Waghana, Angola na wengine tunajiona tuna ukoo na kina kafu! Ronaldo. Hizi tabia ndo zetu na wala hatuna haja ya kujiuliza ni kwanini hatuioni timu yetu ikishiriki katika kombe kubwa kama hili japo mara moja.

Tushiriki ya nini bwana kama watu kombe lilishaletwa tena lile orijinali na tukapiga nalo picha na kisha rais akalibeba kuonesha kwamba sisi si wageni katika suala zima la kabumbu.

najua tumejigawa lakini swali tunalopaswa kujiuliza ni nini tunajifunza kwa kombe hili ukizingatia timu kama Angola inashiriki na kuvitoa jasho vigogo! Tanzania ni nchi ya amani lakini haipendeza kuona ndani ya amani hakuna nafasi ya kujitangaza na sasa soka licha ya kutoa ajira ila ni utalii tosha na nchi kupata wawekezaji katika sekta mbalimbali

Nilitaka kusahau mimi ninashabikia timu hya Ghana na nikiwa kama mchezaji wa soka nafasi ya kiungo mzuiaji na mara mojamoja kufunga ninapendezwa na uchezaji wa Essien, wewe unashabikia timu gani ukiacha Brazil ambayo ni timu ya wote

Furahia michuano mikubwa hii ukijiuliza utafanya nini Tanzania nasi tuweze kushiriki japo raundi ya kwanza

No comments: