Sunday, June 11, 2006

UCHAGUZI MASO-MNMA UMEKWISHA!!!!!!!!

Mpenzi msomaji wa gazeti hili, juma lililokwisha nilikueleza kuhusu mchakato wa uchaguzi wa serikali ya wanafunzi katika chuo cha kumbukumbu ya mwalimu Nyerere, uchaguzi ulifanyika siku ya ijumaa kuanzia saa kumi jioni na mpaka kufikia saa 12 jioni kazi ya kupiga kura ikawa imemalizika wakasubiriwa mawakala waanze kuhesabu kura 'kula'

nafikiri unajua kuwa nilikuwa ni mmoja wa wagombea nikigombea nafasi ya uwaziri wa habari (usishangae hapa MASO uwaziri unagombea, hawateuliwi yaani wote ni kama maraisi) na nilikuwa na nashindania nafasi hii na mtangazaji wa television Zanzibar.

katika uchaguzi huu nafasi zilizokuwa na ushindani mkali ni nafasi ya urais ambayo ilikuwa na wagombea watatu akiwamo mwanamke mmoja pekee aliyejitokeza ( Anna Senkoro!!!) na vivyo hivyo kwa nafasi ya ukatibu mkuu na makamu wa rais (mtu mmoja anakuwa na cheo chenye nyadhifa mbili).

Upande wa nafasi za mawaziri wizara zilizoshuhudia upinzani mkali ni wizara ya michezo na mahusiano ya nje pamoja na wizara ya afya na kafteria.

Najua unadhani nilishindwa na ndio maaana nazunguka tu bila kukupa matokeo hususani ya wizara niliyogombea.

hakuna kitu kizuri kama kusoma ishara za nyakati na kuzifuata, usipozitii basi yatakayokukuta unaweza ukatafuta wachawi na sababu chekwa huku wapiga kura wakiwa pembeni na tabasamu zito wakikuangalia jinsi unavyohangaika kutafuta chanzo cha wewe kushindwa.

Mpinzani wangu, dada mrembo anayepaka rangi ya shaba nywele zake huku tabasamu tamu likiwa usoni kwake kwa wale anaowafahamu alisoma alama za nyakati na akaona hakika hata angeingia katika mbio hizo basi ingekuwa mashindano ya chui na kobe ambapo mshindi anajulikana.

Siku ya mwisho kabisa alijitoa na nikawa mgombea pekee na ushindi nilioupata siwezi kuuita wa tsunami kwani janga hili linaendana na maafa ila tambua kwamba nilipata ushindi mtamu na ni kura 11tu zilimchagua'mwenzangu' na hizi ni kura mhuhimu kwani zinanifanya nijitambue mimi ni nani na ninapaswa kufanya nini si kwa wale walionichagua tu bali kwa wale muhimu wachache walioamua kutekeleza haki yao ya kidemokrasia kwa kupiga kura kwa mpinzani (niruhusu nmwite kivuli)

Bado tunasubiri nafasi moja kwani wagombea katika nafasi katibu mkuu na makamu wa rais hawakufikisha nusu ya kura ili mshindi aamuliwe na hivyo uchaguzi wao jumanne jioni

Tegemea mazuri katika mchakato huu mapema kwani nitakuletea orodha ya wagombea na kura zao.

tafadhari kumbuka gazeti hili sasa liko chini ya wazir wa Habari-MASO

No comments: