Thursday, October 18, 2007

HE! ETI KISWAHILI SIO LUGHA YA WASOMI!!!??


Kama kuna siku niliyoshangaa basi ni siku ya Alhamisi, tukiwa katika mjadala hapa darasani, nilizuiwa kuchangia mada kwa kuwa tu nilipaswa kuongea kiingereza. Nilikumbushwa kuwa lugha rasmi ya mawasiliano katika vyuo vya elimu ya juu ni kizungu na eti Kiswahili ambacho ni lugha ya taifa huru la Tanzania hakina nafasi kwa wasomi wasiosoma lugha hii kama somo.

Wengi walishangaa, niliamua kukaa na mwenyekiti alinionya kutoongea lugha hii tena, na hasa ninapokuwa darasani. Mwisho sana mhadhiri wa somo alisimama na kuniruhusu kuchangia mawazo yangu katika mada iliyowasilishwa na kundi la pili iliyohusu 'ulinganifu kati mitizamo ya kisiasa mmoja ukiwa ni mtazamo kongwe na mtazamo wa kisasa'

Kikubwa ninachopaswa kuwauliza ninyi wengine ni hiki, Je Kiswahili si lugha ya mawasiliano katika sehemu za elimu ya juu? au ndo nimuamini yule mzazi kule kwetu anayajua kwamba kama huwezi kuongea kizungu wewe si msomi, tena nikakumbushwa tu kuwa Kiswahili si chochote na halafu tunapaswa tujifunze Kichina

No comments: