Thursday, October 18, 2007

MAADHIMISHO YA KIFO CHA NYERERE

Juzi chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere kimeungana na watanzania wote kuadhimisha miaka nane tangu kufariki kwa kiongozi wa kwanza wa taifa hili, Mwalimu Julius Nyerere. Sherehe zilikuwa nzuri na zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa chama na serikali akiwamo wazri Kingunge Ngomale Mwiru aliyekuwa mgeni maalum hapa chuoni.

Yaliongewa mengi na tukaoneshwa mengi kuhusu malimu, hakuna aliyepingana nayo. Mada mbalimbali zilizoandaliwa na wahadhiri na wanafunzi zilitolewa katika maadhimisho haya yaliyofanyika kwa siku mbili. Wachangiaji mbalimbali walichangia hii yote ikiwa ni katika kuonesha kuwa kila mmoja anamtambua na kumthamini mwalimu.

Tatizo langu linakuja pale tu wale tuliowategemea kumwonesha mwalimu kama kiongozi wa watanzania wanamwonyesha kama kiongozi wa CCM. Kingunge pamoja na dhamana aliyokuja nayo ya mtumishi wa umma alishindwa kujizuia kutamba kuwa mwalimu ni wa CCM pekee na wanasiasa wanaomwiga wanafanya makosa kwani wao si wanasisisemu.

Kikubwa pia kilichonitatiza ni pale iliposemwa kuwa mwalimu alijali mali na wananchi, hapa naona ni kama tunadanganyana mchana kabisa, ni kweli kwamba mwalimu alijali wanacnhi kwa kutogawa maliasili za nchi.

Wale wanaojidai kuwa mwalimu ni wao leo tunawaona wakiongoza kwa kuuza nchi na utajiri wake, tazama mikataba mibovu inavyosainiwa kila kukicha na pia angalia jinsi mwananchi wa kawaida anavyotaabika kwa bidhaa kuwa ghali huku viongozi na watoto wao wanavyotanua kutokana na kuendekeza matumbo kuliko watu.

Si busara kumuenzi mwalimu kwa kuimba nyimbo zake huku mkicheza ngoma za ubinafsi, ufisadi na mabaya mengine mengi ambayo ni mwiba kwa watanzania, sanamu tu hazitoshi kuonesha kuwa tunamjali mwalimu bali tukumbuke kuwa mwalimu aliona na kuheshimu mali za watanzania na hakutaka kuzitumia kwa manufaa yake binafsi

No comments: