Saturday, September 30, 2006

KUMBE WATANZANIA TUNATUMIKISHA WATOTO!!!

Baada ya Sauper kutuonyesha jinsi tunavyokula samaki mabaki, rais alipiga sana kelele na kuungwa mkono na kila mtu ambaye kwake Darwin9tmare ilikuwa ni uongo kwa kuwa tu kasema raia namba moja.

Sasa kuna hii filam ya IRIN inayoitwa GEM SLAVES Tanzania's Child Labour yaani kwa kiswahili rahisi "utumikishwaji wa watoto katika migodi" filam hii imechukuliwa huko Mirerani wakionyeshwa wanaapollo na 'nyoka' wakifanya kazi ngumu za kutafuta tanzanite wasiyofaidika nayo.

Tumezoea kuandamana na sasa tuusubiri wakazi wa A-town waende barabarani kuilaani filam hii. na cha mno tusubiri rais atakapoenda kuongea na wazee wa arusha atasema nini, kwa kuwa atakachosema kitakuwa ni sahihi kwa watu wanaofikiri kwamba atakalosema ndilo sahii basi tujiandae kuunga mkono hata kama hatujaiona filam yenyewe kama ilivyokuwa kwa wale 'wazalendo' wa mwanza walioandamana kumpinga Sauper bila kuiona hata 'mapanki' yenyewe

No comments: