Monday, October 09, 2006

CHUO KIMEPATWA MSIBA!!!!!

Ni asubuhi ya tarehe 09/10/2006 kilamwanachuoamekwisha jiandaa tayari kwakwenda darasani,mara rais wa serikali ya wanafunzi wa chuocha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere ndugu Hassan J. Masoud anaitisha kikao na wanafunzi wote katika ukumbi wa mikutano.

Hili si jambo la kawaida kwani inaashiria kuna kitu kikubwa wanachuo wanapaswa wahabarishwe, naam, maskio ya kila mmoja yanasubiri nini kitasemwa pale ukumbini na kila mtu yupo kimya. Rais anaanza kuongea ni tangazo la msiba, Msiba mzito wa kaimu naibu mkuu wa chuo ndugu O. K. Temwende

Ni majonzi chuoni na kila mtu haamini kwamba mtu waliyekuwa naye siku moja kabla ametutoka. Kila mmoja anasema analojua na aliloona, wengi tuliongea naye siku ya ijumaa kuhusu tatizo la ada, wengine wakawa naye katika bar ya chuo.

Najua wapo wengi wanaoweza kusema mengi juu ya mwanataaluma huyu, nami pia kwa muda wa kama mwaka mzima tangu nijuane naye chuoni nina mengi yakukumbuka na kujiuliza na kama si kukilaum kifo kwa ukatili uliofanya juu ya mwanazuoni huyu na kada mwaminifu wa chama cha mapinduzi.

Temwende alisoma shule ya Ndanda sekondari zamani sana ikiwa chini ya wabenediktini wa Ndanda shule ambayo miaka ya 90 ilichukuliwa na serikali ambapo nami nilipata elimu ya juu ya sekondari miaka ya 2000. Alipata elimu ya juu katika vyuo mbalimbali vya ndani na nje ya nchi na ninachoweza kukumbuka ni pale alipokwendakuchukua masomo ya juu katika moja ya nchi zakisosharist akiwa na A. Mrema kada mwingine wa CCM enzi hizo ambaye sasa ni Rais wa TLP

Darasani marehemu Temwende atakumbukwa kwa kuwa muwazi na siku zote alisistiza umakini na kushirikiana katika shughuli za kimasomo, alisikiliza tatizo la kila mmoja na hakusita kutoa ushauri kwa yeyote aliyeuhitaji.

Marehemu Temwende aliyezaliwa mkoa wa Mttwara alikuwa ni mwandishi mzuri wa makala na kwa wasomaji wa magazeti na hususani wasomaji wa magazeti ya propaganda ya CCM watakumbuka makala zake nzito zilizokuwa zikitolewa wakati Tanzania ilikuwa katika kipindi cha kusaka maoni uwepo wa vyama vingi katika nchi hii.

Temwende alikuwa na dhamana kubwa hapa chuoni na jinalake litabaki katika kumbukumbu za chuo kwani ni yeye aliyeongoza jopo la wahadhiri wa MNMA katika mchakato wa kukifanya chuo kuwa chuo kikuu na hivyo kutoa shahada. Alifanikiwa na matunda yake hakuna anayeyatilia shaka kwani yanaonekana. Alikuwa ni mtu wa vitendo kuliko porojo na propaganda zisizozalisha.

Kuna mengi ya kuandika juu ya marehemu Temwende aliyefariki wakati akiwa njiani kupelekwa hospitali baada ya kuugua ghafla na kukosa pumzi akiwa nyumbani kwake maeneo ya kigamboni jirani tu na ofisi zake za kazi.

Imetangazwa tuna mapumziko ya msiba lakini mambo aliyoyanya marehemu juu ya chuo na kwa kila mmoja aliyemzunguka hayatafutika na hata wengine kujilamu kwamba kwanini amekubali kufa kama padri Karugendo alivyomlaum profesa S. Chachage kwa kufa ilhali kazi waliyokuwa wameipanga kuifanya haijakamilika na kwa kuwa maisha yanaendelea, kila mtu baadaye atakuwa na furaha na pale Temwende alipokomea basi ndipo tutakapoanzia.

Bwana Alitoa na Bwana Ametwaa

Pumzika kwa Amani mpendwa wetu Omar K. Temwende

1 comment:

Anonymous said...

machweo.blogspot.com is very informative. The article is very professionally written. I enjoy reading machweo.blogspot.com every day.
bad credit personal loans
canada payday loans