Sunday, October 29, 2006

MRAMBA, BILA MWALIMU, NYERERE NI MTU MWINGINE


Hivi karibuni waziri Mramba aliutangazia umma wa watanzania kuhusu madiliko katika kiwanja cha kimataifa cha dar es salaam. mabadiliko hayo ni katika sehemu moja muhimu sana nayo ni ya utambulisho wa mgeni kujua hapa ni wapi na mwenyeji kujivuna kwa kuwa na utambulisho huo.

Mramba na timu yake wanasema kwamba kutokana na sababu za taratibu za kimawasiliano, kiwanja cha ndege cha dar maarufu kama Mwalimu Nyerere international airport sasa kitakuwa kinaitwa Nyerere IA.

mmmh! hii kweli ndo kasi mpya inayohubri mabadiliko makubwa kwa watanzania na mabadiliko haya ndiyo tunayoyaona sasa, yaani watu kwa utashi wao tu wanaamua kubadili jina la kiwanja hiki kwa kuwa tu wazungu hawawezi kutamka jina mwalimu!

Huu ni ulimbukeni na kama anavyosema msanii wa parapanda Mputo katika ghani zake 'salamu zangu' kuwa msikihubiri kiswahili kwa kukitukuza kingereza, kwani kwa miaka yote jina la nyerere shurti lianze na mwalimu na hapo kila mtu duniani hatohoji kwamba huyu mwalimu ni nani. Alijulikana dunia nzima na harakati zake zinazofundishwa kila kona ya dunia hii.

Kuondoa jina mwalimu kisa tu kuna wachache wanapata shida kutamka ni sawa na kusema JFK IA libadilishwe na kuwa unavyotaka wewe. Mbona kuna majina ya viwanja vya ndege si Africa tu bali na sehemu mbalimbali duniani ni magumu si kutamka tu bali hata kuandikwa lakini ndiyo yanayobeba viwanja hivyo.

wanamachweo wanategemea waziri na wizara yake itafanya kama watanzania wanavyohitaji bila kuhoji kwa nini!

na kwa kumalizia kwa watu wenye mawazo kama ya Mramba ni kwamba huwezi kusema nyerere ukimaanisha mwl Nyerere tunayemfahamu sisi watanzania na watu wote duniani, labda kama mnataka kutueleza kuwa jina hilo halina maana sasa.

No comments: