Thursday, March 09, 2006

MWANA 'MASO' BLOGU HII NDILO GAZETI LAKO, LITUMIE




Ni jambo la kushangaza kwamba jumuia ya chuo hiki kilichobeba jina la baba wa taifa la Tanzania Mwl. J. K. Nyerere hakina gazeti la wanachuo. Kila mwenye mawazo yake timamu atajiuliza na kupata jibu lazima awatafute wahusika, nimewatafuta na jibu kutoka kasso halieleweki

Si kwamba hawajui maaana ya gazeti kwa wanachuo la, ni uzembe na mazoea ya labda kwa kuwa library kuna Mtanzania na Rai, Daily Newz na hivi wanachuo wanapaswa wasome na si kuchangia hoja zao katika gazeti lao.

Kwa kuona tatizo hili ninakuomba mwanachuo mwenzangu tumia blogu hii kutoa maoni yako ya aina yoyote ilmradi tu haumtukani yeyote. Tumia lugha yoyote ila ningependa sana kama ukatumia Kiswahili ili na wengine wengi wanaojua maana ya lugha hii katika kuwasiliana wakasoma na kufurahi, kuongeza uelewa na kushiriki katika mijadala mbalimbali ninayoitegemea kutoka kwako.

Nina imani kabisa hata serikali ya wanachuo itakuwa na nafasi ya kuchangia na kueleza yote yanayojitokeza ofisini kwao. Najua matangazo yao mengi wanayatoa kwa kuandikwa kwa mkono lakini kwa kuwa chuo kitaendesha kozi ya kompyuta basi natumaini hali itabadilika na pale ubaoni hatutaona tena tangazo lililoandikwa kwa mkono toka Administration na katika serikali ya wanachuo.

nakukaribisha sana katika blogu hii jisikie huru kutoa mawazo yako yenye kujenga jamii nzima si ya wanachuo tu bali ya wasomaji wote wa ndani na nje ya nchi kwani ni ukweli kwamba blogu haina mipaka na kazi ya kuihariri inahitaji busara ya kutembea na taa mchana

No comments: