Sunday, March 19, 2006

Wow! Nmerudi tena. Baada ya kimya kifupi, sasa ninakuja tena na kitu kipya na cha kawaida kabisa kwenye higher institution kama hii ya kwetu. Wiki kesho tunaanza mitihani ya kwa ajili ya term ya pili kwa mwakahuu. Ninachukia mitihani lakini ndo hivyo tena kwani hakuna maana ya kusoma kama hujaribiwi kwa kile ulichokisoma.
Nawajua wengi amabo kila wakisikia mitihani baaasi kuumwa si kuumwa na kila kitu kinabadilika yaani wanaweza kusahau hata kuoga.
Ninachukia mitihani lakini si kama ninaiogopa, la , siwezi kuiogopa kwangu mtihani mgumu kabisa ulikuwa ni wa darasa la nne ambapo kila mwanafunzi kipindi kile alikuwa na kitete cha kuingia darasa la tano. Siidharau mitihani hii ila ni kwamba ninataka kuwaencourage watahiniwa wenzangu kwamba kama wao waliomaliza walifaulu kwa nini sisi tushindwe,
Nawatakia mitihani mizuri na mfanye mkiwa na moyo wa kijiamini. Love

No comments: