Saturday, April 15, 2006

ILIKUWA NI TERM YA FURAHA!!!

Wow! Kwa mara ya kwanza!

Barua ya Kaimu Mkuu wa Chuo cha MNMA ilibandikwa ubaoni ikitoa 'shavu' kwa Mr O. K. Temwende ( Kaimu Naibu wa Mkuu wa MNMA) na kamati yake ya taaluma kwa kufanikisha utaratibu wa chuo kuanza kutoa B.A. Mara zote tunajua wakubwa hupongezana ndani kwa ndani na wakati mwingine mkubwa sana hampongezi mdogo na hatambui mchango wake lakini kwa mara ya kwanza barua ya Dk Magotti inasomwa na kila mtu na wote tunakubali na kuithamini kazi ya Mr Temwende. Bravo Mr Temwende na kamati yako!

Wanachuo wote tunapewa vitambulisho vizuri kabisa ( sina uhakika na ubora wake hususani ile nailoni kuachia na kufanya karatasi kuchanika! nakumbuka jinsi dean of student alivyochachalika kuhakikisha vijana wake tunatembea tukiwa tunatambulika,( unamkumbuka yule jamaa wa SS1 aliyesema kwamba alikamatwa na polisi kitambulisho cha kuazimia vitabu maktaba kikamuokoa! Alikuwa anatoka kuwachangia tbl kuwafanya watoe kodi kubwa kwa serikali na mishahara minono kwa wafanyakazi wakitukutanisha pamoja bushtrekker tehetehete!

Hivi tangazokwamba kuna mafunzo ya kompyuta linatuhusu wote

No comments: