Thursday, February 01, 2007

KUKOSEKANA KWA HUDUMA ZA KOMPYUTA CHUONI KUNA SABABISHA USUMBUFU KWA WANAFUNZI......

Unashangaa kuona kichwa hicho, najua unategemea kabisa hili kutokuwa tatizo katika chuo tena cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere. Umekosea.

wakati shule zinazoitwa za 'academy' (sio academy ya mwalimu nyerere) siku hizi watoto wanafundishwa kompyuta, hali hii ni tatizo hapa chuoni kwani ukitaka kufahamu ni wanachuo wangapi wana uwezo wa kutumia kompyuta basi idadi yao itakusikitisha na kukufanya labda ufikiri kuwa hapa kumejaa ubabaishaji tu.

Sio kwamba kompyuta hakuna, la, zipo kama 40 lakini zima ndani ya vyumba vyenye milango ya chuma na mlinzi nje kuhakikisha kuwa hakuna anayechungulia na kuona vitu vya ajabu, kompyuta.

Mkuu kateuliwa na labda tunaweza kuanza kuiona kompyuta 'live'

Tungoje na kwa wale wasiojua basi wasubiri au waende wakajiandikishe katika akademia za kitoto

No comments: