Thursday, February 01, 2007

KAULA TENA!!!

Kila mmoja alikuwa na mshawasha wa kutaka kujua ni nani atashika nafasi ya ukuu wa chuo cha kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, wengi walikuwa wakifikiria mabadiliko......

Majuzi waziri wa elimu ya juu kafanya kile ambacho alipaswa akifanye, kuteua mkuu wa chuo nafasi ambayo ilikuwa inashikiliwa na daktari Magotti ambaye pia ni kada mkubwa chama tawala CCM.

Uteuzi umefanyika na aliyeteuliwa kuwa mkuu wa chuo ni yuleyule aliyekuwa akikaimu na ambaye amekuwa mkuu wa chuo tangu kilipokuwa chuo cha chama na sasa chini ya serikali.

Ndiyo, jina jipya la chuo lakini mkuu yuleyule, hii ina maanisha kuwa tutegemee mengi na makubwa toka kwa kiongozi mkongwe.

machweo inamtakia dr Magotti kazi njema na itampa ushirikiano wa kutosha kama tulivyoombwa na msarifu ambaye naye ana kaimu nafasi hii, kwa maoni yetu sisi wana machweo tunadhani hata msarifu arudishwe yuleyule na pia korando likarabatiwe liwe jipya.

No comments: