Thursday, December 28, 2006

UNAFIKI WA WAANDISHI KTK KUPONGEZA MWAKA MMOJA WA KIKWETE MADARAKANI


Naaam, rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania JMK ametimiza mwaka mmoja tangu watanzania wamuamini katika kuwaongoza.
Mwaka mmoja si kipindi kizuri cha kuamua na kutoa tathmini ya kilichofanya na mtu tunayetegemea atuongoze kwa miaka mitano.
Waandishi wengi sana wamejitokeza kutoa na kuelezea mafaniko ya rais ndani ya mwaka huu mmoja, kila mmoja amemsifu na hii ni haki yake.
Tunajua kabisa rais amekuwa ni kipenzi cha waandishi wengi tangu enzi za mchakato wa uchaguzi na mpaka anakuwa rais, kwa hali hii si rahisi kwa watu waliokuwa wakimtukuza kama mtu mwajibikaji kuanza kumtenga na kueleza uhalisia.

Kwa upande wangu mimi sioni mafanikio yoyote kama baadhi ya waandishi wanavyotaka kutuaminisha na vyombo vyao, tazama hali ya usafiri kwa wakazi wa Kigamboni jirani kabisa na ikulu, siwezi kuyaona mafanikio ya kodi tunazoambiwa zinakusanywa kwa mabilioni wakati hakuna pantoni la uhakika, au hawa waandishi wanataka tufe baharini na waandike habari za kiongozi kuja kuwatembela ndugu zetu.

Hizi sifa anazopea JMK ziangaliwe tena kwani hakuna mabadiliko yoyote

No comments: