Monday, December 04, 2006

WASOMI WETU NA MIKATABA FEKI


Usiogope. Nadhani unakumbuka enzi za akina chifu Mangungo wa msovero na lile jasusi la kijerumani Karl Peters, enzi hizo watawala wetu walilazimishwa na kulazimika kusaini mikataba feki iliyowafanya wapoteze tawala zao katika nchi walizokuwa wanazitawala.

Kuna sababu nyingi zilizowanya wasaini mikataba hii, moja kubwa ikiwa ni ile hali ya kujua kusoma na kuandika lugha za kigeni. pamoja na kusaini mikataba hii feki watawala hawa wa kiafrika walikuwa wakichukua muda kuijadili na kuifikiri mikiataba hii.

Tofauti na sasa ambapo watu tuliowaamini katika kuongoza nchi yetu tajiri yenye watu wapole na wakarimu, ndio wanaotuumiza na kutufanya tukae gizani kwa kuingia mikataba ya kutunyanyasa huku wao wakifaidi 'aksante' waliyopewa na mambazi haya.

Fikiria mikataba yote ambayo serikali yetu imesaini, fikiria ile ya madini, IPTL na sasa huu mpya wa sijui inaitwa Richmond, hivi mikataba hii inamsaidia nini mtanzania wa kawaida. Ninasema wa kawaida kwa sababu sasa watanzania tunatofautiana, tuna matabaka yaani ni kama nchi za kibepali.

Mikataba hii walioisaini wapo, tunawajua na wanaendelea kula kuku tu na huku wakituimbia nyimbo za kutukaririsha ya kuwa uchumi wetu unakua! unakua au unakuwa!

Mimi si mchumi lakini siamini ukuaji wa uchumi huku nchi ikiwa haina umeme wa uhakika, ni mgao tu kwa kwenda mbele huku wale tuliowaamini kutuwakilisha bungeni wanakaa kimya na kujadili mambo hata yenye jibu tayari, wanajadili eti kuhusu vazi la spika, inamaana spika yuko uchi au wanadhani wakimnunulia spika vazi jipya ndipo watajadili hoja tunazotaka wazijadiliili.

Kwanza hilojoho akilifua atalinyoosha na nini? OOOps nilisahau kumbe wao ni tofauti na mimi, wao kila siku ni full kipupwe, full kiyoyozii

No comments: