Saturday, December 23, 2006

HE!!! INAWEZEKANA.......

Juzi tumekuwa na kikao na mshauri wa wanafunzi (mwaka wa pili) kikao kilikuwa na mabo mengi yaliyoongelewa kikubwa ikiwa ni masuala mbalimbali ambayo wanachuo tunaona hayaeleki kwa kuwa hayajawekwa wazi na uongozi, kwa mfano suala la ada pamoja na utafiti , inakuwaje tunatoa pesa nyingi kila mwaka wakati utafiti tunaufanya kwa mwaka mmoja tu, pia tunalipa kodi kubwa ya pango (21000/=)kila mwezi ilhali huduma katika hosteli ni mbovu hususani ubovu wa makabati na upungufu wa matundu ya vyoo, hebuchukulia mfanowa hosteli ya Kizota juu ambayo inawakaazi karibu 70 lakini wote hawa wanategemea matundu mawili ya vyoo pamoja na milango minne ya mabafu!
Huduma ya chakula inatolewa na mtu mmoja tu, kwanini, ina maana hakuna watu wengine wa kutoa huduma kwa wanafunzi hasa ukizingatia kuwa mtoa huduma huyu hatoi huduma zinazoendana na namba ya wanachuo! Nani katika menejimenti anamlinda,kwanini serikaliya wanafunzi inasema kuhusu tatizo hili na blahblah toka kwa utawala ndo zinatawala!

Usiogope! haya yalijibiwa na mshauri ambaye kwa kweli alijitahidi sana kupunguza jazba za washikadau!
Hii ndo hali halisi iliyopo hapa chuoni na labda tutegemee mabadiliko kwani ukarabati uliochukua muda mrefu kuliko ujenzi ndo kwanza upo katika hatua za mwisho huku sisi wanachuo tukikosa maktaba na hivyo kufanya masomo yetu kuwa magumu hasa ukizingatia kuwa kutegemea maktaba za nje ni ghali kwa mabo ya kivuko ambacho kinachukua muda mrefu kuvusha watu huku ratiba ikiwa inatukaba kwa sana. Hii yote tisa ni hili lililotokea mkutanoni lilianza hivi...

baada ya dean kutoa nafasi kwa wanachuo kuuliza maswali na kutoa yote yanayowakereketa, akasimama mwanadada wa kozi ya Gender anaitwa dada Agnes, huyu ni mlemavu wa macho, haoni na kwa hapa chuoni yupo peke yake.

Aliposimama kuongea kila mtu ukumbini alinyamaza ili kusikiliza nini anasema, akiongea kwa sauti inayosikika masikioni kwa uzuri kabisa aliyatoa yake mengi na hasa lile ambalo yeye analiona kwamba kuwepo kwake hapa chuoni kumekuwa ni mzigo na inawezekana kwa kuwa chuo kimemuona ni mzigo kimeshindwa kuwapa nafasi walemavu kama yeye walioomba nafasi za masomo chuoni.

Yeye anakabiliwa na matatizo mengi katika kujisomea kwani gharama zote zinamwangukia yeye na chuo kinashindwa kumsaidia japo kwa kumtafutia karatasi za kuandikia. Alijaribu kuwapatia management anuani za mashirika ambayo yanawasaidia watu wenye matatizo kama yake lakini anashangaa hakuna chochote kilichoendelea, hajapata msaada.

Wote tulinyamaza na sikia jibu hili toka kwa Dean "si kweli kwamba chuo kinakuona wewe kama mzigo, kinajivunia kuwa nawe hapa na hata huwa naona wageni wanapotutembelea hapa huelezwa kuwepo kwako hapa". Naam, tulishukuru kwamba mshauri mwenyewe aliahidi kumsaidia dada huyu ili aweze kufanikisha kile kilichomleta hapa na kumwelewesha kwamba chuo hakina noma na kuwepo kwake hasa ukizingatia vyuo vyenyewe ndo hivi tu.

Kikao hakijaisha, nitakuwa nikikutaarifu kadri siku zinavyokuja kwani kuna fukuto ambalo linahitaji majibu na kwa hulka ya 'wakubwa' labda wanasubiri kitendo kitokee ndipo waseme wanavyoona ni sahihi kwa wanachuo kufanya

No comments: