Monday, December 18, 2006

LONGOLONGO ZA RICHMOND! KUNA 'WAKUBWA' HAPO

Mmeyasikia wenyewe, hakuna haja ya kuyarudia kuyaandika malumbano yanyoendelea kati ya shirika la ugavi la tanesco na 'wasanii' wanaojiita richmond. Hawa waliingia mkataba wa kuzalisha megawati 100 za umeme kwa kutumia majenereta yao waliyotoa marikani na kuiuzia tanesko. mitambo iliwasili na baada ya mbwembe nyingi sana za kuahidi kuzalisha kwanza megawati 20 kabla ya tarehe 1desemba2006 huku wakisaidiwa na waziri wa nishati, hakuna umeme uliozalishwa.
Sasa wamekuja na longolongo ya kusema kwamba eti tanesco imewapatia gesi chafu yenye kokoto! ukiniambia gesi kuwa na kokoto kwangu mimi nitakushangaa, hivi kumbe gesi ina kokoto kama zile za kujengea zege!
bado ninalia na wale wote waliofunga mkataba na kampuni hili linalodai lina makazi yake marekani huku mwakilishi wake hapa akiwa na mkoba tu, huu ni usanii

Hivi JK anasubiri nini kuwawajibisha wanasiasa waliosani mkataba huu, wakati mwingine ninajiuliza kama waziri mkuu alikuwa na sababu ya kulijibu shairi la bwana Marwa akijitapa kuwaonesha viongozi waadilifu waliojaa tele hapa nchini, yaani wamejaa tele halafu wafunge mikataba mibovu kama hii na bado waendelee kuwa wasafi na waliojaa tele.

Jeshi la polisi lipewe kazi ya kuwasaka wote 'waliojaa tele' na kusaini mkataba huu ili wafikishwe mahakamani na sheria ichukue mkondo wake! (unakumbuka enzi za kufilisiwa)

majambazi yakikamatwa basi tv zitarusha sana ama kibaka akiwa mikononi mwa wanachi wenye hasira, kila mmoja hunyanyua mkono ili amwadhibu kibaka lakini majambazi ya peni hapa kwetu yana heshimika sana na wanaonekana mahujaa, naamini kabisa richmond wamekula na 'waliojaa tele' na wanaendelea kutanua katika magari yenye viyoyozi kwani tarehe za pcb ni nyingi kurekebisha na kuua so.
Kaeni kimya mkisubiri uongo mwingine toka kwa wasanii wa Richmond

No comments: