Saturday, December 23, 2006

Miaka 45 ya uhuru: viongozi huru wenye suti za kikoloni

Naam, sherehe za kuadhimisha miaka 45 ya uhuru wa Tanzania (ipi ilipata uhuru, Tanganyika au Tanzania!) zimemalizika na kamati imevunjwa huku waziri mkuu akijipanga tena kuongea na wafanyabiashara ili wasaidie katika maandalizi ya sherehe zijazo.

Sherehe hizi zimefanyika kama kumbukumbu kuadhimisha uhuru wan chi yetu toka kwa wakoloni, waingereza ambao walipewa jukumu la kuwa waangalizi (Tanganyika became the british protectorate) wan chi yetu kwani Un haikuwa watawala na mnamo tarehe 9desemba 1961 bendera ya malkia ikashushwa na bendera yenye rangi nne kumaanisha Tanzania ikapandishwa.

Miaka 45 si mingi sanakwa miaka uhai wa taifa japo si haba kujivunia miaka hii tukiwa huru, na kwa kufikisha miaka hii hakuna haja ya kuacha kusheherekea kwa mbwembwe na majivuno mengi kuonesha ni nini maana ya kuwa huru.

Kusheherekea uhuru ni jambo muhimu sana yaani ni kama mtu wa kawaida anaadhimisha ‘birtday’ yake. Uhuru unamaanisha hali na uwezo wa kujiamulia mabo yako bila kuingiliwa na nchi au taifa jingine (sovereignity).

Sherehe za mwaka huu zimekuwa tofauti kidogo na zile zilizokuwa zikifanywa na wamu zilizopita. Hizi zilikuwa ni za ari mpya, nguvu mpya na ari mpya.

Zimekuwa ni tofauti kwa maana ya kwamba hizi zimeendana na mkesha wa nguvu uliooneshwa moja kwa moja na luninga ya taifa (TVT). Hii iliwapa nafasi watanzania wote kushuhudia sherhe hizi zilizoambatana na tatizo la kukatika katika kwa umeme..

Suala la kukatika kwa umeme siyo ishu iliyonishawishi na kunivuta kuandika kuhusu maadhimisho haya. Na wala sitaongelea suala la waziri mkuu kuwaomba wafanyabiashara wakubwa wajitokeze kuchangia na kufanikisha sherehe hizi zinazokadiliwa kugharimu bilioni moja na ushee pesa za kitanzania.

Wengi wameongelea kuhusu sherhe hizi, wapo waliohoji kuhusu suala la ni nchi gani iliyopata uhuru, mwandishi nizar visram yeye anashangazwa na tukio la waziri mkuu kukutana na wafanyabiashara ili wafanikishe sherehe hizi, kwake hili ni kama kuibinafsisha siku muhimu kwa watanzania wote.

Wanasosolojia nao hawakuwa kimya katika kuadhimisha shehere hizi zilizoshuhudia kwa mara ya kwanza madege yetu ya kivita yakipita kwa mbwembwe kusherehekea siku hii muhimu, wao wamehoji kuhusu ni nani hasa anayesheherekea siku hii kwa watanzania. Kwao matabaka yanayojitokeza nchini yanawafanya wahoji je ni kweli sherehe hizi ni za wote au ni kwa baadhi ya watanzania? Haya yameongelewa na si vibaya kuyajadili katika nchi hii inayoadhimisha miaka 45 ya uhuruhuju pengo kati ya maskini likiwa linaonekana wazi, maendeleo ya mijini na vijijini yakiwa na tofauti kubwa na huku mipango ya maendeleo vijijini ikijadiliwa na watu wa mjini.

Sasa turudi kwenye mada kwani isije nikaonekana nataka tu kujaza kurasa, lakini hata hayo niliyoyagusa ni muhimu yakajadiliwa na pia yatatuongoza katika kutambua mada ya leo.

Mavazi ni kitambulisho kikubwa cha uataifa wa mtu kama zilivyo pesa, wimbo wa taifa pamoja na ramani ya nchi. Leo hii ukiangalia nchi huru nyingine za kiafrika utaweza kuwatambua raia wan chi hizi kwa kuyaangalia mavazi wanayovaa, hebu chukua mfano wan chi za Nigeria, Ghana na afrika kusini. Tanzania na uhuru wetu bado hatuna vazi letu la taifa.
Katika mkesha wa kukaribisha saa sita,pale mnazi mmoja, wote tutakuwa mashahidi kwa namna viongozi wetu walivyokuwa wamependeza katika mavazi mazuri ya gharama toka magharibi. Kwa kifupi mavazi hasa yaliyokuwa yamevaliwa na viongozi yalikuwa ni kama tunaadhimisha uhuru wa nchi moja ya kimagharibi.


Tumeshuhudia umati wa watanzania waliohudhuria mkesha huu wakiwa na mavazi ya aina tofauti, huku wengi wasio jukwaani wakiwa ndani ya mavazi yaliyo kwenye ‘chati’ kwa sasa miongoni mwa watu wa chini ‘mitumba’.

Huku mkesha ukiambatana na ulipuaji wa baruti, tumeshuhudia viongozi wetu waliokuwa wakishuka toka katika magari makubwa nay a gharama wakiwa ndani ya suti nzito na za gharama. Tumeshudia viongozi wanaume wakiwa ndani ya suti nzito toka kwa wabunifu wa kimagharibi, mavazi ambayo yanaonesha kabisa kwamba inawezekana tukawa tunajitawala kwa kufikiri na kuvaa kimagharibi! Angalau mavazi yaliyokuwa yamevaliwa na wanawake viongozi yalijaribu kuonesha utamaduni wa kiafrika kwa kuuvaa Unaijeria na Ughana.

Kwa maisha ya leo yawezekana kabisa baadhi ya watu wakaona suala la mavazi ni ishu ndogo sana kiasi cha kujadiliwa katika kuadhimisha miaka 45 ya uhuru wan chi yetu. Kwangu hili ni suala la kujadili kwani kujitawala ni pamoja na kuonesha waliotutawala kwamba sasa sisi tuko huru yaani tunaweza hata kuwa na maamuzi katika mavazi ya kuvaa.

Uhuru una maana nyingi sana ikiwa ni pamoja na kuonesha hali ya kuwa na maamuzi katika utamaduni wako unaoongoza maisha yako ya kila siku. Mavazi ni sehemu ya utamaduni.
Utamaduni ni zaidi ya ngoma tunazozishudia zikialikwa kutumbuiza katika sherehe hizi. Ngoma kwa sasa kwa baadhi ya watu zimekuwa zikionesha ukale, kinachotamba sasa ni utamaduni wa ‘bongo fleva’. Tumeshuhudia kila mara vikundi vya ngoma vilipokuwa jukwaani havikupata mapokezi mazuri toka kwa hadhira lakini pale walipopanda ‘wanaume tmk’ wakiwa wamevaa mavazi ya kisasa kelele za kushangilia zililipuka. Huu ndio utamaduni tunaoushabikia sasa na miaka 45 ya uhuru.


Mwandishi mahiri katika suala la utamaduni wa mwafrika, mwanazuoni Kihumbi Thairu (the African Civilization) anawashangaa wale wote wanaodharau mavazi yetu na kukumbatia mavazi ya kigeni yasyojali hali ya hewa na mazingira ya nchi zetu za kiafrika. Mavazi haya ya kigeni tunayoyavaa sit u kwamba yanashindwa kututambulisha sisi ni kina nani bali yanatufanya tukose sababu ya kusheherekea uhuru wan chi yetu.

Kwa jinsi kila kitu kilivyokuwa kikifanyika pale mnazi mmoja huku kila mmoja akiwa katika vazi lake ni uthibitisho tosha kwamba kwa sasa tuko huru kweli kweli na mwingereza hana chake tena..

Jukwaa zima lilikuwa limetawaliwa na mavazi ambayo hayakuonesha maana ya kusheherekea uhuru wetu. Miaka 45 ya kujitawala ni mingi sana kuweza kujiamulia ni nini tunapenda kuvaa, baadhi yetutumechagua kuuvaa umagharibi ndani ya umaskini wa uhuru.
Natambua juhudi zilizofanywa na baadhi ya watu waliokuwa na mapenzi ya kutupatia watanzania kitambulisho kwa kubuni vazi la taifa. Hii ilikuwa nikipindi cha miaka ya 2000 na ninakumbuka kwamba baadhi ya wabunifu walifika mpaka kule Dodoma nyumbani kwa bunge la watanzania.


Kama ilivyo kawaida ya waswahili ‘watu wa ahadi’ suala hili sasa hakuna anayeliongelea na hata vazi lililoshinda nadhani sasa litakuwa limepambwa makumbusho kwa ajili ya kuvionesha vizazi vjavyo kwamba hili ni vazi la kitanzania ambalo halikuwavaliwa kwani wazazi wao walikuwa wakivaa mavazi mengine kwa kuwa tu walikuwa huru, wenye uwezo wa kujiamlia mabo yao wenyewe bila kuongozwa na mtu mwingine.

Kwangu mimi tofauti niliyoiona katika upande wa mavazi ina maanisha vitu vingi sana ikiwemo suala la kuibuka kwa matabaka katika jamii yetu. Matabaka ambayo yanashindwa kuelewa maana ya uhuru wa nchi yetu.

Mika hii 45 ya uhuru na mavazi yaliyovaliwa na wakati wa sherehe hizi na hasa yale ya viongozi wetu yanaonesha kabisa kuwa sasa uhuru wetu umekuwa ni kwa ajili ya kuchangisha pesa toka kwa wafanyabiashara wakubwa ili kufanikisha sherehe hizi ambapo mtanzania wa kawaida anaishia kukesha akiwa amevaa mavazi yasiyoeleka hasa mitumba huku viongozi wakijichana wakiwa ndani ya suti nzito zilizobuniwa na wabunifu toka kwa wale tuliokuwatukiwaita wakoloni na mabeberu.

Kwa kuona kwamba katika sherehe hizi hakuna aliyekuwa uchi, basi sula la vazi la taifa si muhimu hasa ukizingatia kuwa nchi yetu na utawala huu una mambo mengi ya kuonesha sasa tuko huru. Kila mmoja amevaa nguo anayoitaka na kumudu kununua kutokana na ruhusa ya kipato chake. Kwa kuwa na mambo mengi ya kuleta maisha bora kwa kila mtanzania suala la mavazi si la kujadili kwa sasa

No comments: