Saturday, May 06, 2006

KOMPYUTA NDANI YA MILANGO YA CHUMA!!!!!!

Ndugu msomaji nimeamua kuipandisha kurasa hii ambayo niliiandika mwaka jana wakati chuo hiki kikiwa hakina huduma acha ya kompyuta kwa wanafunzi bali hata mtandao kwa ajili ya kuwasaidia katika kutafuta 'material' kulingana na kozi wanazosoma.

Hali sasa ni tofauti kwani milango ya chuma sasa imefunguliwa na kompyuta zipo huku wasimamizi wa maktaba wakiwepo kusaidia wale wote wanaotatizwa na teknolojia hii. Haya ni mabadiliko na tunajua kuna mengi yanakuja. hebu soma nilichoandika kipindi hicho ambacho leo ni historia


Ukifika na kuuliza ni hakika utaambiwa wanachuo wanasoma kompyuta kwani ni kweli kabisa kuna madarasa mawili yaliyojaa kompyuta na bahati nzuri nyingine zimeunganishwa katika intanet. Majibu utakayopewa ukaridhika na upande mmoja basi ukweli halisi huwezi kuupata na utaondoka ukiwa na furaha ya kwamba kweli chuo kimebeba jina linalostahili hivyo nacho kinastahili.

Labda nikuonyeshe upande wa pili wa majibu uatakayoyapata kutoka kwa walengwa wenyewe, wanachuo. Hakuna mafunzo ya komyuta na hakuna mwanachuo anayeruhusiwa wacha kuzigusa kompyuta zenyewe bali hata kusogelea karibu a milango miwili ni shida, milango yote inalindwa na mageti ya chuma na kufuli maalum yaani kama za benki.

Inashangaza sana kwa chuo kama hiki kutowaruhusu wanafunzi kutumia vifaa hivi kwa ajili yua kujisomea na kufanya kazi nyingine za kitaaluma kwani hakuna ubishi kwamba intaneti inamwezesha msomaji kusoma vitabu vingi na vya wakati huu.

Juzi nimekutana na rafiki yangu namfahamu tangu tukiwa A-level, yupo hapa chuoni na alikuwa library akitafuta kitabu cha Rural Sociology ambacho hakipo katika 'shefu' za maktaba, alisikitika na nikamwona akimjongea mhusika wa library kujaribu kumwomba agoogle' apate japo nini cha kusoma

Hii haipendezi na hasa kama mtu mzima anapohubiri mabadiliko bila kubadilika akitegemea anaowahubiria wabadilike! Inawezekana tu kama wanaohubiriwa wataamua kumbadilisha yeye kwanza na bila kujali watatumia nini kumbadilisha

Nadhani ujumbe huu ni salamu tosha kabisa kwa MASO kutambua kwamba wapo kama daraja la kutusemea sisis tunataka nini, na si kukaa tu wakilipana posho kwa pesa tunazokatwa kama ada ya chama

Pia uongozi hasa kamati ya taaluma ambayo naamini kabisa inaongozwa na mtu anayependa wanafunzi wajifunze vizuri katika mazingira rafiki uatalifikiria jambo
hili

No comments: