Tuesday, May 23, 2006

WALIOCHELEWA WAMESAMEHEWA!!!!!!!!!


Juzi nilikuandikia kuhusu suala la wanachuo wachache waliokuwa wamechelewa na chuo kupitia kwa dean! wakaamriwa wafukuzwe na kama watapenda basi warudia mwaka wa masomo.

Wengi wa hawa waliochelewa ni wanafunzi wa mwaka wa pili ambao ni kama wamebakiza siku 26 wamaliza kozi na kutunukiwa diploma yao kama watakuwa wamefaulu.

Mapema leo asubuhi wamepewa barua za kuondoshwa chuoni zikiwa zimesainiwa na kaimu wa naibu wa mkuu wa chuo.Barua hizo hazina rejea hata moja na kuonyesha kosa la mhusika, zimemshangaza kila mmoja hata yule asiyekuwa na elimu ya sheria kifupi ni kwamba zinakanganya sana.

mkanyiko huu hauishii kwenye barua tu kwani wakati wa kipindi cha tatu leo mchana Naibu wa mkuu wa chuo hiki cha Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere, aliwaita wahanga wa msala huu na kuwasamehe, tena kwa msamaa usio na barua.

Inachanganya kuona kwamba mtu umemfukuza kwa barua na unamrudisha kwa kutompa barua, hii haina matatizo ya kisheriakweli au ndo mtindo wa mazoea kwamba mimi ndo kila kitu na ninachosema ndicho kifanywe hata kama kuna bodi yenye dhamana ya chuo hiki

No comments: