Tuesday, May 23, 2006

UCHAGUZI BILA KATIBA!!!

Usije ukafikiri ninachokuandikia hapa ni utani. 'Kaimu' rais wa MASO ametoa tangazo la kuwataka wale wote wanaotaka kuingia katika mchakato wa uchaguzi wa serikali ya wanafunzi hapa chuoni basi wachukue fomu katika ofisi za MASO!

Kila mmoja maeliona tangazo hilo lenye sahihi tu ya rais bila muhuri wa MASO yaani kwa ufupi kama usipokuwa makini tangazo limekaa kama barua tu unayoweza kumwandikia shangazi yako. Kila mtu anajiuliza hivi kweli uongozi hauna muhuri na kama hauna muhuri na kama hauna basi huu ni uhuni na haupaswi kuwepo.

No comments: