Wednesday, May 24, 2006

Jamani, nimekuwa nikiwaza na kuwazua; Ni nani mfanyakazi bora katika ofisi zetu Tanzania?

Nauliza hivi kwa kuwa kila ifikapo tarehe kama ya leo kila mwaka, ofisi huwa zinahaha kutangaza wafanyakazi bora. Sijui wanatumia vigezo vipi.
Muda wote wachapakazi ndo wanakosa nafasi hizo na wanaopata ni wale wanaopendwa na wanaowateua; iwe manajimenti, ofisa mtendaji mkuu na wote wanaofanana na hao.
Sasa mimi nasema hakuna cha mfanyakazi bora wala nini. Wote n i watumishi tu na mtindo huo wa kuwepo wafanyakazi bora unadumaza utendaji wa kazi wa watu wengine na ndiyo maana nchi zetu haziendelei.
Nimemaliza

No comments: