Saturday, August 05, 2006

MAKAHABA TUWAFUKUZE, AU TUWAPE MITAJI WASITEGEMEE MIILI YAO?

Swali hili linatokana na hatua aliyoichukua mkuu mpya wa mkoa wa Dar es salaam bwana Kandoro.
Mkuu huyu baada ya kupewa rungu la ukuu wa mkoa muhimu wa kibiashara nchini tanzania alikimbilia maeneo ya manzese uwanja wa fisi na kuwatimua mabinti wadogo wanaofanya biashara ya kuuza miili (yeye anaiita ukahaba).

Siungani na watu wanaoshabikia kuwepo kwa mabinti hawa maeneo haya kwani licha ya kuwa umalaya/ukahaba si kitu kizuri kwa dunia ya sasa yenye gonjwa la ukimwi lakini wengi wa mabinti hawa ni wasichana wadogo kiumri(wengi wako chini ya miaka 18 miaka ambayo ni ya mtoto kuwa shule akitafuta elimu).

Sasa wamefukuzwa maeneo haya na wengine wamefikishwa mahakamani ambako mahakama imewaachia kwa kuwaona kuwa hawana hatia (ushahidi ni mgumu zaidi ya kumfungulia mtu mashtaka ya uzururaji). Kwa maana hiyo mabinti hawa wamefukuzwa toka maeneo yao na kutakiwa waondoke kwenda haieleweki wapi na wakafanye nini kwani sasa hawatakiwikujihusisha na umalaya/ukahaba tena.

Sielewi kama mkuu wa mkoa alikuwa anatafuta jina katika kurasa za mbele za magazeti yetu ama ni kasi mpya na nguvu mpya!

Unaweza kujadili suala hili, je kuwafukuza hapo ndilo suruhisha au suluhisho ni kuwaandalia mbiu nyingine za maisha kama KIWOHEDE wanavyofanya pale Buguruni. Pia ni lazima jamii ijue kuwa si Uwanja wa Fisi tu kunakofanyika uchafu huu, ni sehemu nyingi sana hapa dar na katikamiji mikubwa mingine kama Mwanza, Mbeya na Arusha

No comments: