Saturday, August 05, 2006

KANDORO NA WAKAZI WA MABONDENI NANI ZAIDI

Wakati akiwaapisha wakuu wapya wa wilaya za jiji la dar aliwataka kuhakikisha kuwa wanafanya kazi zao na kutimiza wajibu wao kwa mujibu wa katiba. Huu kila mmoja anauelewa ili alinde kitumbua chake

Lakini amewakasirisha wakazi wa mabondeni ambao wamekuwa ni sugu na mara zote wameishinda serikali mahakamani kuhusu suala la kutoka katika maeneo haya hatari hususani maeneo ya jangwani.

Kilichonifanya niandike jambo hili ni ile kauli ya wakazi wa jangwani kwanza kumhusu Kandoro kama yeye na yeye kama mkuu wa mkoa, jiji la dar

Wengi walimweleza kama mgeni ambaye hata mjini hajakaa halafu anaanza kuwaletea longolongo wakati wao wamekuwa pale kwa miongo na watoto wao wanasoma muhimbili primary huku wakipata huduma ya uhakika ya matibabu toka hospitali ya taifa Muhimbili halafu leo Kandoro apange kuwaondoa!

Mgosi (Makamba) kashindwa atakuja yeye! tusubiri tuone kwani kasi aliyokuja nayo ya kuwatimua mabinti pale uwanja wa fisi inaweza kuwa juu ya wakazi wa mabondeni

No comments: