Tuesday, July 25, 2006

KILA MTU NI MPIGADEBE!

Hata wewe ni mpigadebe
Haya kaandika mwandishi makini wa makala katika gazeti la kila wiki RAI, huyu ni faza Priva Karugendo, nisipoteze kusema alichosema hebu soma mwenyewe na uone alivyoandika na kwa kauli yake hatakomea hapokwani ataandika mengi kuhusu hili(wakati anaandika alikuwa anawahi ndege toka mwanza kuja dar, huyu ni mwanaharakati wa mambo ya kijamii, na mwanafalsafa wa kileo,ukisoma makala yake anayomlaumu Chachage kwa kufa utaelewa ninachokisema) na hivyo usiache kusoma suala hili katika blog hii

Ndugu yangu, Asante sana kuandika. Leo hii nitakuwa Dar. NitaondokaMwanza, na ndege ya saa mbili usiku.Ukipata nafasi uniite kwenye simu. Lakini Juma lote nitakuwa ninakimbia huku na kule. Unajua, Watanzania wote ni wapigadebe! Maana yake ni kwamba: Hatufanyi uzalishaji. Mtu ananunua shati Kampala, analileta Magu, Mwingine ananunua shati lilele na kulipeleka Mwanza, wa Mwanza, analipeleka Moshi, Arusha hadi Dar. Yote hayo ni sawa na kupiga Debe. Mpigadebe, anapata pesa kwa kumleta mtu kwenye gari, ambalo hata kipofu anaweza kujua kwamba linaelekea Mwanza! Anapata pesa bila kuzalisha chochote. Mwisho wa mwezi anakuwa na pesa kuwazidi watu walioajiriwa ofisini!

Umeyaona haya, mengi yaja

No comments: