Tuesday, July 25, 2006

WAPIGADEBE

Nimeamua nichokoze mawazo yako wewe mwananchi kuhusu suala la wapigadebe katika vituo vya mabasi ya ndani ya miji (daladala kwa dar na express kwa mwanza)na nje ya miji (yale yaendayo mikoani)

Hawa ni vijana wenye umri wa kati kuanzia miaka 15 hadi45 yaani ni kama marehemu profesa Chachage alivyopenda kuwaita vijana wa kizazi cha dot.com. Aliwaita hivi kwa sababu moja kubwa bayo ni kwamba wengi wa vijana wamezaliwa baada ya tz kupata uhuru yaani baada ya 1961 na wamekulia katika kipindi ambacho nchi imeshuhudia mabadiliko makubwa ya kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni,

Tukirudi kwenye mjadala kuhusu kundi hili ambalo sasa linakua kwa kasi mpya na nguvu ya jumbo, hivi ni sababu zipi zinasababisha hali hii itokee

Je jamii inahusika na jamii ni nani kama ni hivyo! serikali na taasisi zake ina mkono katika hili!

karibu utoe maoni yako!

No comments: