Thursday, July 06, 2006

TUMEFUNGA CHUO!!!

Ijumaa iliyopita ilikuwa ni siku muhimu sana kwa wote wanachuo kwani ukiacha wengine waliokuwa wanamaliza mwaka wao wa kwanza wa masomo wengine walikuwa wakimaliza kozi zao za stashahada na cheti.

Ilikuwa ni siku ya maagano huku kila mmoja akiwa na huzuni ya kuachana na rafiki yake na furaha ya kupokea cheti na kuanza mwaka mpya wa masomo bila kusahau ada iliyopanda

Blogu hii inawatakia mapumziko mema wanachuo wa vyuo vyote na ni wajibu wetu kutunza afya

No comments: