Wednesday, July 12, 2006

PROFESA CHACHAGE KATUTOKA!!!!

Hakika nakosa maneno ya kuandika kuhusu kifo cha ghafla cha guru la midahalo ya kisomi kuhusu masuala mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.

Inahitaji kuwa na nafasi kubwa kuweza kuandika kile ninachofahamu kuhusu mtaalam huyu wa sayansi ya jamii na mwandishi wa vitabu.

Nakikumbuka kitabu chake ambacho kinapingana na utandawazi usio haki unaopigiwa chapuo na viongozi ambao nia yao si ya jamii nzima bali ni kujitajirisha peke yao na watoto wao, kitabu hicho kinaitwa Makuwadi wa Soko Huria

Si kwamba watanzania tumepoteza lulu bali afrika nzima na wote wanotaka usawa duniani wamepoteza hazina kubwa lakini kupitia maandiko na machapisho yake hakika watazaliwa kina chachage elfu

Nakumbuka msemo wako wakati ukihojiwa na mtayarishaji wa kipindi cha luninga Sema Usikike ulisema neno ambalo sitokaa nilisahau " hakika kuhusu ujambazi kuna sehemu imeoza na wala si sahihi kusema kwamba umaskini ndo chanzo cha ujambazi, jamii na viongozi wa serikali wajiangalie wapi kuna mgogoro unaozalisha wimbi la majambazi na wapiga debe"

Buriani Pro. Seithy Chachage

No comments: