Saturday, March 17, 2007

ETI TIMU YA MNMA KAMA 'ASENO'

Ni jana tu ambapo wanachuo walishuhudia timu yao ya mpira wa miguu ikicheza na timu ya vijana wa mtaani wanaojulikana kama 'nantes' timu ambayo mfadhili wake mkuu inaaminiwa ni mhasibu wa chuo cha kumbukumbu ya mwalimu nyerere ndugu Magulumengi.

Ikicheza kitimu timu ya chuo ilikukuwa ya kwanza kuliona lango la wapinzani wao kupitia kwa mfungaji wake makini Magesa aliyefunga bao tamu baada ya kupata pasi safi toka kwa kiungo mfungaji Marijani.

Bao hilo liliwafanya wageni wachanganyikiwe huku kiungo wa nantes Dinno akihangaika kuipita ngome ya chuo iliyokuwa chini ya ulinzi wa dogo Allan. Hadi kipindi cha kwanza kinakwisha chuo walikuwa wakiongoza kwa goli moja.

Kipindi cha pili timu ya wageni ilifanya mabadiliko yaliyosaidia kupatikana kwa goli la kusawazisha lililofungwa dakika 20 baada ya kipindi cha pili. Bao hili liliwaduwaza chuo na kujikuta wakicheza bila mpangilio na mabeki wakicheza faulo zilizosababisha chuo kufungwa goli la pili. faulo iliyopigwa dakika za majeruhi pembeni mwa lango la timu ya chuo ilizaa goli lililowaduwaza wachezaji na mashabiki wa chuo kwani licha ya kuwa timu yao ilifungwa bali lilimaanisha uteja wa kudumu kwani tangu 2005 timu ya chuo haijawahi kuwafunga vijana wa nantes ambao huongozwa na kapteni mwenye maneno mengi Ben Shoo.

Pamoja na mabdiliko makubwa yaliyofanywa na chuo ya kuwaingizi Chidi, Munga na seki timu ya chuo ililala na kumwacha mshabiki ambaye hujifanya kocha hanzuruni akiapa kutoshangilia tena timu ambayo haina dhamana.

Mashabiki walioongea na mwandishi wa blog hii walionekana kukerwa na kufungwa huku na wakaifananisha timu yao kama timu ya aseno ambayo mbali na kucheza mpira na kuumiliki kwa muda mrefu alkini wamejikuta hawana chao msimu huu.

No comments: