Thursday, March 08, 2007

SIKU YA WANAWAKE DUNIANI!
JAMII IWAANGALIE WANAWAKE WAJAWAZITO!!!

Nimeamua kuandika waraka huu nia kubwa ikiwa ni kutaka kukuonesha wewe msomaji adha wanayoipata wanawake wengi wa Kitanzania hasa wanapokuwa wajawazito. Wanawake wajawazito hasa wale wa vijijini wanapata wakati mgumu sana na unaoogopesha pindi wanapokuwa wakifuata huduma ya 'kujifungua' katika hospitali za serikali.

Hospitali nyingi za serikali zimekuwa si rafiki wa wajawazito hasa wale wanaotoka vijijini ambako umaskini humsabahi kila mtu katika nchi hii inayohubiri maisha bora kwa kila mtanzania. Wanapofika hospitali wanalazimika kununua mahitaji ya kupatiwa huduma ilhali serikali imetangaza kuwa 'vifaa' hivi hupatikana bure kwa wote, hii si kweli.

Wanahitajika kujinunulia vifaa hivi ambavyo kwao ni ghali sana na wengine huamua kabisa kuacha kwenda hospitali kwani masaibu watakayokutana nayo huko yanatisha.

Kuna baadhi ya hospitali, tena nyingine zipo mijini kabisa kina mama wajawazito wamekuwa wakirundikwa wodini kama magunia ya viazi, huku kitanda kimoja kikilaliwa na wajawazito wawili 'wenye bahati' na wasiona bahati basi wasubiri saa katika sakafu.
Ni serikali yenye jukumu la kuhakikisha kuwa hospitali zake zina si huduma bora na vifaa tu bali wahudumu wapo wa kutosha na wanaowezestoa huduma kwa kila mmoja bila kujali hali ya kipato chake.

Leo tunapoungana na wanawake kushehereke siku yao duniani ni jukumu la kila mwanajamii na serikali kujiuliza wanawake wajawazito wanasaidiwa vipi

No comments: