Wednesday, March 07, 2007

HATA BLOG HII INABADILIKA!!!!

Msomaji wa machweo, nimekuwa nikikuandikia kuhusu mabadiliko makubwa yanayoendelea hapa chuoni ikiwa ni pamoja na mabadiliko ya jina la chuo cha kumbukumbu ya nyerere mpaka kuteuliwa kwa viongozi wa kuongoza chuo na kubwa zaidi maktaba ya kompyuta kuanza kutumika.

Kwa mabadiliko haya, nami pamoja na waandaaji wa blog hii tunajipanga ili kuiboresha blog hii ivutie na pia kuongeza 'utamu' kwako msomaji.

Kwa sasa unapofungua blog pembeni utaona viunganishi ambapo utaweza kutembelea blog nyingine za kiswahili ikiwemo ya Ndesanjo, Mkina, Ngurumo na ile ya katuni za Kipanya.

Mengi yanakuja nami nawaahidi kuwapa kile mnachoona kinafaa, tafadhari msisite kutuma maoni yenu katika blog hii

No comments: