Friday, March 02, 2007

NI MABADILIKO TU KILA KONA, UMEYAONA MASHANGINGI...

Leo imekuwa ni siku njema na ya furaha sana kwa walioteuliwa kushika nyadhifa hapa chuoni, kama huna habari ya uteuzi huu ngoja nikupashe kidogo. Juma lililopita bodi ya chuo chini ya m/kiti dr Salim A. Salim iliwateua ndugu Mushi na ndugu Luambano kushika nyadhifa za juu kabisa hapa chuoni, Mushi aliteuliwa kuwa naibu wa mkuu wa chuo na Luambano kuwa msajiri wa chuo, hii imekuwa ni habari njema kwao.

Licha ya uteuzi kumaanisha 'posho' kuongezeka na majukumu tele lakini uteuzi huo umeendana na kuletwa kwa 'mashangingi' magari mazuri ya kifahari (sema ya anasa) ili kurahisisha utendaji kazi wa vionngozi hawa.

Jumuia tumeombwa kutoa ushirikiano kwao lakini hatujaona sehemu wao walipoombwa kutoa ushirikiano kwetu, labda tutapata lifti! Tusubiri tuone

No comments: