Thursday, March 08, 2007

LEO NI SIKU YA WANAWAKE DUNIANI!!!!

Wanawake duniani kote leo tarehe 8mwezi wa 3 wanaungana wote duniani kutambua siku yao. Jamii nyingi duniani zinawachukulia wanawake kama binadamu wa 'pili' huku wanaume wakiwa ni wa kwanza bila kujali mchango mkubwa unaoletwa na wanawake katika suala zima la kuleta maendeleo kwa taifa na familia kwa ujumla.

wanawake ni muhimu sana kwa taifa kwani ukiachana na jukumu lao kubwa la kuongeza 'wanachama' katika taifa, wamekuwa ni mstari wa mbela katika kujenga jamii bora kabisa kwa kujenga misingi imara ya tabia za watoto na hivyo kuwa kichocheo kikuu cha maendeleo ya jamii.

Jamii zetu kwa sasa zimebadilika sana katika suala la kumtambua na kumthamini mwanamke, hapo zamani mwanamke alikuwa anabaguliwa na familia katika suala zima la elimu lakini kwa sasa hali ni tofauti kwa uwezo wao mkubwa darasani na mawazo yao endelevu vimechangia kujenga misingi madhubuti katika nyanja ya elimu. Kwa nchi kama tanzania, wasichana miaka miwili mfululizo wamekuwa wakiongoza katika matokeo ya mitihani ya kidato cha nne na sita. Hii imeongeza changamoto kwa jamii kuona kuwa mtoto wa kike anafaa sana kusomeshwa na kama ule usemi wa msomi maarufu unaosema 'kumwelimisha mwanamke ni kuelimisha jamii' unatimia

1 comment:

Anonymous said...

Good words.