Wednesday, March 28, 2007

KANISA LILISHIRIKI UTUMWA!!!

Niliyofundishwa kwamba walipokuja wamisionari hawakuja kufundisha juu ya Mungu, walikuja kushiriki kikamilifu ili kuhakikisha kwamba wazungu wanapata watumwa kwa namna yoyote ile. Walikuja wakiwa wameshika baibo na wakakiri kabisa kwamba wao ni wema na mungu wao anaruhusu utumwa.

Usishangae! Majuzi kanisa la Angilikana limekubali na kusikitishwa na kitendo chake cha kushiriki katika biashara 'haramu kwa kipindi hiki' halali ya utumwa kwa kipindi kile. Akiongea mjini Landani jumamosi wakati wa maandamano ya kuadhimisha miaka200 tangu bunge la Uingereza lilipopitisha sheria ya kuzuia biashara na utumwa wenyewe, askofu mkuu wa canterbury daktari Rowan Williams alisema kwamba kanisa linasikitishwa na hali ile na linapanga kulipa fidia.

Swali, Watamlipa nani

No comments: