Wednesday, March 21, 2007

NINI KINAMBEBA 'MTOTO WA MJINI'!!!

Unaikumbuka ile kesi ya wale jamaa waliomuua wakili Kapinga mnamo mwaka2002! Jamaa hawa walikaa rumande kwa muda wa miaka5 na hukumu ya kesi ilitaja kuwa walikuwa wakituhumiwa kumuua wakili huyo maarufu. Hawa hawakuonwa. Dito kaua hadharana na bado kamanda wa polisi anajaribu kutuaminisha kuwa bastola ilivyatuka kwa bahati mbaya! Amefanikiwa kwani mapema tu DPP aliibadili kesi toka mauaji mpaka kukusudia kuua.

Mahabusu wengi wenye kesi za namna ya 'mtoto wa mjini' wamekaa rumande kwa muda mrefu sana kwa kuwa tu 'upelelezi haujakamilika' (hawa si matajiri) jiulize jamaa waliotuhumiwa kumuua Kapinga hawakuona na yeyote lakini mahakama imewahukumu hukumu nzito kabisa. Dito, hadharani kabisa katoka ndani ya shangingi lake kashika bastola na kuifyatua ikimlenga dereva bado tunaambiwa eti hakukusudia kuua! Tunakokwenda siko.

Jiulize waziri mmoja anasimama na kusema kuwa kesi ya kigogo huyo imekuwa hivyo kwa sababu ana mawakili wazuri! mawakili wazuri ama kuna kitu kingine kilichoanzia kwa Tibaigana, mkurugenzi wa mashtaka na 'serikali'

Tunakokwenda siko na itafikia wakati wenye kutosikia watasikia na mabubu watasema, nimalize kwa kukumegea kipande ambacho mwanamuziki na mwanaharakati Tracy Chapman anasema katika wimbo wake 'Revolution'. Utafute na uusikilize utapata zaidi ya sauti nzuri na milio murua ya magitaa (mara nyingi hutumia gitaa tu)

No comments: